Waziri wa Madini Mhe Doto Biteko (Mb) akijibu swali bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 5 Novemba 2019 wakati wa mkutano wa kumi na saba.
Waziri wa Madini Mhe Doto Biteko (Mb) akijibu swali bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 5 Novemba 2019 wakati wa mkutano wa kumi na saba.
Serikali kupitia wizara ya Madini
imehakikishia wananchi mkoani Mra kuwa itawalipa fidia wananchi wote
waliohakikiwa kwa ajili ya kupisha mgodi
Waziri wa Madini Mhe Doto Biteko
ameyasema hayo leo tarehe 5 Novemba 2019 bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali
la Mbunge wa Viti Maalum mkoani Mara Mhe Agness Marwa aliyetaka kufahamu ni
lini mgodi wa Acacia uliopo Nyamongo utalipa fidia kwa wananchi.
Amesema kuwa Serikali imeendelea kusimamia Sekta ya Madini kwa
kuhakikisha Uwekezaji unafanyika kwa mujibu wa Sheria na Taratibu za Nchi
ikiwemo kuhakikisha kuwa wananchi wanaoishi katika maeneo ambayo miradi ya uendelezaji
migodi inataka kufanyika na kulazimika kupisha maeneo yao, wanalipwa fidia
stahiki kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi na wanapewa makazi mbadala ambayo yana
hali bora kuliko makazi waliyokuwa nayo awali.
Mhe Biteko aliongeza
kuwa Uthaminishaji katika
maeneo yanayozunguka mgodi wa
North Mara na ulipaji wa fidia umegawanyika katika awamu nyingi kwa
kuzingatia vijiji husika kuridhia. Kijiji cha Nyabirama chenye wakazi 1,974 waliothaminiwa
katika awamu ya 20, 35 na 42 wote walilipwa fedha zao isipokuwa wakazi 64 ambao
fidia yao iliyoidhinishwa ya shilingi bilioni 1.9 waliikataa na hundi zao zilibaki
Ofisi ya Mkurugenzi wa Wilaya ya Tarime. Eneo la Kijiji cha Nyabichune lilithaminiwa katika awamu ya 47 na
kuidhinishwa shilingi millioni 224 kwa ajili ya
watu 69. Wizara iliagiza uthamini wa maeneo ya kijiji cha Nyabichune urudiwe
kwa sababu wananchi walipunjwa.
Amesema, Mthamini Mkuu wa Serikali ameshakamilisha uthaminishaji kwenye maeneo 1,838 ambapo tayari ameshawasilisha
kwenye menejimenti ya mgodi kwa hatua
zake za ulipaji.
Aidha, Kuhusiana na suala la mgodi kubadilisha aina ya uchimbaji toka
uchimbaji wa wazi (open pit) kwenda underground mining, uamuzi huo ulifikiwa
baada ya mgodi kufanya utafiti ulioonesha kuwa gharama ya uchimbaji wa chini (underground mining) ilikuwa ni ndogo
ukilinganisha na gharama za kuendelea na mgodi wa wazi.
Mhe Biteko amewatoa shaka wananci wa Tarime kuwa Wizara inafuatilia kwa
karibu uchimbaji unaofanyika na mpaka sasa uchimbaji wa underground unafanyika eneo la Gokona kuelekea Nyabigena ndani ya
maeneo waliyokuwa wakichimba tangu awali. Hivyo, hakuna eneo ambalo mgodi wa underground unachimba kwenye makazi ya
watu.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment