Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe (Mb)
akijibu swali bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 6 Novemba 2019 wakati
wa mkutano wa kumi na saba
Na
Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali
inatambua umuhimu wa kuwekeza katika mazao mbalimbali ya kilimo yakiwemo mazao
ya viungo ambayo mahitaji yake yanaendelea kuongezeka ndani na nje ya nchi.
Kwa
kutambua umuhimu huo, Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania
(TARI) imeanza kufanya utafiti wa kupata mbegu bora za mazao ya viungo na mazao
mengine ya bustani (Horticulture) ili
kuongeza uzalishaji na tija.
Naibu
Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe ameyasema hayo leo tarehe 6 Novemba 2019 bungeni
Jijini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa jimbo la Mkinga Mhe Dunstan
Luka Kitandula aliyetaka kufahamu kama Serikali ipo tayari kuwawezesha wakulima
hao kupata mbegu bora ili waweze kuongeza uzalishaji wa mazao yao.
Amesema
kuwa Serikali kupitia Wizara ya Kilimo inapitia Sera ya Kilimo ya Mwaka 2013
ambapo sekta ndogo ya mazao ya bustani (horticulture) ni miongoni mwa maeneo
muhimu yanayozingatiwa. Vilievile, kutokana na umuhimu wa mazao ya horticulture, Serikali kupia Wizara ya
Kilimo itafanya kikao cha wadau wa mazao hayo tarehe 8 Novemba, 2019 ili
kuandaa Mkakati wa Miaka Mitano wa Kuendeleza Mazao ya Bustani.
Mkakati huo unalenga
kuongeza uzalishaji, ubora wa mazao, kuimarisha mifumo ya masoko ya mazao hayo.
Aidha mkakati huo utakuwa ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa
unaolenga Taifa letu kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025.
Aidha,
pamoja na hatua hizo, Mhe Bashe ameongeza kuwa Serikali inaendelea kutoa elimu
ya kilimo bora cha mazao ya viungo, uhifadhi, usindikaji na masoko kwa
kushirikiana na Sekta Binafsi kikiwemo Chama cha Wadau wa Mazao ya Viungo
Tanzania (Tanzania Spices Association –
TASPA), Sustainable Agriculture
Tanzania (SAT) na vyama vingine vya wakulima.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment