METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, November 30, 2019

Mamluki katika Mashindano ya Michezo ya Wafanyakazi kuchukuliwa Hatua


Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akizungumza leo Novemba 30,2019 Jijini Mwanza na Wanamichezo ambao ni wafanyakazi (hawapo pichani) wakati alipofungua mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Mashirika  ya Umma na Binafsi yanayofanyika Jijini humo kuanzia tarehe 27 Novemba hadi 01 Desemba 2019,yanayongozwa na Kauli mbiu “SHIMMUTA 2019 Familia Moja”lengo ikiwa ni kuimarisha afya na kubadilishana uzoefu kazini. Kulia ni Mwenyekiti wa SHIMMUTA Bw. Khamis Mkanachi na Kushoto ni Mkuu wa Wilaya Mhe.Dkt.Fillis Nyimbi.
Mwenyekiti wa SHIMMUTA Taifa Bw.Khamis Mkanachi  akiongea kuhusu SHIMMUTA leo Novemba 30,2019 Jijini Mwanza na Wanamichezo ambao ni wafanyakazi (hawapo pichani) wakati  Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (katikati) alipofungua mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Mashirika  ya Umma na Binafsi yanayofanyika Jijini humo kuanzia tarehe 27 Novemba hadi 01 Desemba 2019,yanayongozwa na Kauli mbiu “SHIMMUTA 2019 Familia Moja”lengo ikiwa ni kuimarisha afya na kubadilishana uzoefu kazini.Kushoto  ni Makamu Mwenyekiti wa SHIMMUTA Bibi Roselyn Massam.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akipiga mpira wa penati  leo Novemba 30,2019 Jijini Mwanza kuashiria ufunguzi wa Mashindano ya Wanamichezo ambao ni wafanyakazi alipofungua mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Mashirika  ya Umma na Binafsi (SHIMMUTA) yanayofanyika Jijini humo kuanzia tarehe 27 Novemba hadi 01 Desemba 2019,yanayongozwa na Kauli mbiu “SHIMMUTA 2019 Familia Moja”lengo ikiwa ni kuimarisha afya na kubadilishana uzoefu kazini.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Bibi Phillis Nyimbi  akitoa salamu za Wilaya na Mkoa leo Novemba 30,2019 Jijini Mwanza  wakati Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (kulia) alipofungua Mashindano ya Wanamichezo ambao ni wafanyakazi  wa Mashirika ya Umma na Binafsi (hawapo pichani yanayofanyika Jijini humo kuanzia tarehe 27 Novemba hadi 01 Desemba 2019,yanayongozwa na Kauli mbiu “SHIMMUTA 2019 Familia Moja”lengo ikiwa ni kuimarisha afya na kubadilishana uzoefu kazini.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa SHIMMUTA Bibi Roselyn Massam.
Bibi Elinaike Naburi ambaye ni Afisa Utumishi kutoka TPDC akiwaapisha wanamichezo wenzake leo Novemba 30,2019 Jijini Mwanza  wakati Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) alipofungua mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Mashirika  ya Umma na Binafsi (SHIMMUTA) yanayofanyika Jijini humo kuanzia tarehe 27 Novemba hadi 01 Desemba 2019,yanayongozwa na Kauli mbiu “SHIMMUTA 2019 Familia Moja”lengo ikiwa ni kuimarisha afya na kubadilishana uzoefu kazini.
Bw.Felix Eliudi ambaye ni Muamuzi akila kiapo kwa niaba ya waamuzi wote watakaochezesha mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Mashirika  ya Umma na Binafsi (SHIMMUTA) yanayofanyika Jijini humo kuanzia tarehe 27 Novemba hadi 01 Desemba 2019,yanayongozwa na Kauli mbiu “SHIMMUTA 2019 Familia Moja”lengo ikiwa ni kuimarisha afya na kubadilishana uzoefu kazini ambayo yamefunguliwa na wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akisalimiana na wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Chuo cha Usimamizi wa Biashara  CBE kampasi ya Mwanza leo Novema 30,2019 mara baada ya kufungua mashindano ya Michezo kwa Wafanyakazi wa Mashirika ya Umma na (SHIMMUTA) yanayofanyika Jijini humo kuanzia tarehe 27 Novemba hadi 01 Desemba 2019,yanayongozwa na Kauli mbiu “SHIMMUTA 2019 Familia Moja”lengo ikiwa ni kuimarisha afya na kubadilishana uzoefu kazini.
………………
Na Shamimu Nyaki –WHUSM ,Mwanza

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe ametangaza kuwachukulia hatua Wanamichezo wasiokuwa Wafanyakazi  maarufu kwa jina la “Mamluki” wanaoshiriki Mashindano ya Michezo kwa  Wafanyakazi inayojulikana kama SHIMUTA na SHIMIWI endapo watabainika.

Dkt.Mwakyembe amesema hayo  leo Jijini Mwanza wakati akifungua michezo ya Mashirika ya Umma  na Binafsi maarufu kwa jina la SHIMMUTA kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluh Hassan ambaye pia ndiye  mlezi wa mashindano hayo ambapo amesema kuwa lengo la mashindano hayo ni kuimarisha afya za wafanyakazi,kubadilishana uzoefu pamoja na kutangaza Taasisi zao.

“Kuna hili suala la Wachezaji ambao sio wafanyakazi maarufu kwa jina la MAMLUKI kushiriki karika michezo hii,tena nakumbuka kuna kiongozi aliwahi kuwaita “viongeza nguvu bambikizi”,Hapa sio mahala pao nawataka wajiondoe mapema maana tukiwabaini wao pamoja na Taasisi zao tutawachukila hatua”alisema Waziri Mwakyembe

Mhe.Waziri Mwakyembe ameongeza kuwa wakati mwaka jana mashindano hayo yalipofanyika Jijini Dodoma  Mhe.Makamu wa Rais Mama Samia hakuridhishwa na idadi ya washiriki kutokana na Idadi ya Makampuni na Mashirika yaliyopo nchini,hivyo kuagiza mkutano ufanyike kujua sababu na kuzipatia majibu ambapo  maazimio yameleta matunda kwani mashindano ya mwaka huu idadi imeongezeka kutoka 26 hadi 46.

Hata hivyo Mhe.Waziri amewataka waamuzi  wa mashindano hayo kuchezesha michezo hiyo kwa haki na kufuata sheria zote za michezo  na atakayesababisha vurugu au masononeko atawajibishwa kupitia kiapo alichoapa leo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa SHIMMUTA Bw.Khamis Mkanachi amesema kuwa Menejimenti za Taasisi za Umma pamoja na Makampuni binafsi zinatakiwa kuelewa kwamba wafanyakazi wao wanatakiwa kufanya michezo mbalimbali ili kuimarisha afya zao kwa ajili ya kuongeza ufanisi wanapokuwa kazini,hivyo ni wajibu wa kila Taasisi na mashirika kuona haja ya  kutenga siku ya kufanya michezo.

“Michezo hii inafanyika kwa mwaka mara moja ni vyema viongozi wa Taasisi na Mashirika binafsi kuona umuhimu huo na kuwapa wafanyakazi wao muda wa kushiriki michezo hiyo inayoleta ari katika kufanya kazi” aliongeza Bw.Mkanachi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt.Fillis Nyimbi amesema Jiji la Mwanza hususan Wilaya ya nyamagana imeshukuru ujio wa mashindano hayo kwakua itaongeza kipato kwa wenyeji kutokana ongezeko la watu waliokuja kwa ajili ya mashindano hayo ambapo pia amewahakikishia amani na usalama.

Vilevile mwanamichezo Eliud Felix kutoka timu ya Jiji la Mwanza amesema michezo hiyo imewasaidia kujuana pamoja na kubadilishana uzoefu wa majukumu ya kila mmoja katika taasisi yake na kupendekeza iendelee kufanyika kila mwaka.

Mashindano hayo yalianza rasmi tarehe 27/11/2019 na yanatarajiwa kumalizika Desemba mosi 2019 ambapo jumla ya Mashirika na Taasisi 46 zimeshiriki ikiwemo wenyeji Ofisi ya Mkoa wa Mwanza,Chuo Kikuu Dodoma,Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na nyingine.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com