METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, October 4, 2019

ZIARA YA MHESHIMIWA WAZIRI MKUU MKOANI SINGIDA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,  akizungumza na Mkandarasi wa mradi wa maji Kintinku/Lusilile, Injinia Jumanne Werema, uliyopo katika Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida, Oktoba 4.2019. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi. Waziri Mkuu yupo mkoani Singida kwa ziara ya kikazi  ya siku nne.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,  akizungumza na Watumishi wa Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida, kwenye ukumbi wa Halmashairi wilayani hapo, Oktoba 4.2019.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,  akiangalia korosho zilizotoka, kwenye mradi wa shamba la korosho la Masigati wilayani Manyoni, wakati alipokagua mradi huo, Oktoba 4.2019. Kutoka kushoto ni Mke wa Waziri Mkuu, Marry Majaliwa na kulia ni Meneja wa Kanda ya Kati, Bodi ya Korosho, Ray Mtangi.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,  akiangalia mti wa korosho, kwenye mradi wa shamba la korosho la Masigati wilayani Manyoni, wakati alipokagua mradi huo, Oktoba 4.2019.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,  akiweka jiwe la msingi wa jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, mkoani Singida, Oktoba 4.2019.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akikagua jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, baada ya kuweka jiwe la msingi wa jengo hilo, Oktoba 4.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com