METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, September 18, 2019

NAIBU SPIKA AZINDUA TULIA TRUST COMPUTER LAB KATIKA SHULE YA SEKONDARI SAMORA MACHEL






Leo Septemba 18, 2019 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson amefanya uzinduzi wa chumba cha Computer kilichopewa jina la TULIA TRUST kilichopo katika Shule ya Sekondari Samora Machel iliyopo mkoani Mbeya ili kuwawezesha Wanafunzi kuweza kujifunza masomo ya computer kwa vitendo ili kuendana na teknolojia iliyopo sasa.

Awali Dkt Tulia aliwezesha shule hiyo kupata Computer tano za kuanzia ambapo pia ameahidi kuwaongezea Computer nyingine pamoja na mashine za kuchapisha mitihani na kutolea copy.

Katika hotuba yake Dkt Tulia amesema ”Kwakweli nimekutana na maajabu makubwa sana kwa hii hatua mliyofikia ya kujenga chumba hiki kizuri na kikubwa ingawa zimetajwa baadhi ya changamoto ikiwemo uchache wa Computer kwakuwa wanafunzi ni wengi, mimi niahidi tu kwamba nitaleta Computer nyingine hapa ili kuweza kumudu idadi ya wanafunzi”

“Nimeelezwa pia watoto wote hapa kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita wanakaa mitaani ambapo ni changamoto kwao, kwenye hili niseme tutatafuta wadau na ikiwezekana tuanze kujenga mabweni kwa ajili ya watoto hawa lakini napenda tuanze na mabweni ya watoto wa kike kwa sababu hawa changamoto zao ni kubwa zaidi ukilinganisha na wakiume ingawa tungetamani tujenge yote hivyo kwa kuanza tutaanzia hapo”- Alisisitiza Dkt Tulia Ackson
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com