Leo Septemba 18, 2019 Naibu Spika wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson amefanya uzinduzi wa
chumba cha Computer kilichopewa jina la TULIA TRUST kilichopo katika Shule ya
Sekondari Samora Machel iliyopo mkoani Mbeya ili kuwawezesha Wanafunzi kuweza
kujifunza masomo ya computer kwa vitendo ili kuendana na teknolojia iliyopo
sasa.
Awali Dkt Tulia aliwezesha shule hiyo
kupata Computer tano za kuanzia ambapo pia ameahidi kuwaongezea Computer
nyingine pamoja na mashine za kuchapisha mitihani na kutolea copy.
Katika hotuba yake Dkt Tulia amesema ”Kwakweli
nimekutana na maajabu makubwa sana kwa hii hatua mliyofikia ya kujenga chumba
hiki kizuri na kikubwa ingawa zimetajwa baadhi ya changamoto ikiwemo uchache wa
Computer kwakuwa wanafunzi ni wengi, mimi niahidi tu kwamba nitaleta Computer
nyingine hapa ili kuweza kumudu idadi ya wanafunzi”
“Nimeelezwa pia watoto wote hapa kuanzia
kidato cha kwanza hadi cha sita wanakaa mitaani ambapo ni changamoto kwao,
kwenye hili niseme tutatafuta wadau na ikiwezekana tuanze kujenga mabweni kwa
ajili ya watoto hawa lakini napenda tuanze na mabweni ya watoto wa kike kwa sababu
hawa changamoto zao ni kubwa zaidi ukilinganisha na wakiume ingawa tungetamani
tujenge yote hivyo kwa kuanza tutaanzia hapo”- Alisisitiza Dkt Tulia Ackson
0 comments:
Post a Comment