METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, August 18, 2019

WANANCHI WA KIJIJI CHA WAMI NA MBUNGE MGIMWA WAIKATAA BARABARA INAYOTENGENEZWA NA KAMPUNI YA FABEC CIVIL AND TELECOM ENGINEERS

Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa akiungana na wananchi kuikataa barabara ambayo inatengenezwa na kampuni ya Fabec civil,Building and Telecom Engineers inayotoka katika kijiji cha Vikula kwenda wami(mbalwe) akiwa na sambamba na diwani wa kata ya Ihalimba Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa akiungana na wananchi kuikataa barabara ambayo inatengenezwa na kampuni ya Fabec civil,Building and Telecom Engineers inayotoka katika kijiji cha Vikula kwenda wami(mbalwe)
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa mbunge wa  jimbo la Mufindi Kaskazini wakimsikiliza mbunge wao juu ya utengenezaji wa barabara unaotekelezwa na kampuni ya Fabec civil,Building and Telecom Engineers inayotoka katika kijiji cha Vikula kwenda wami(mbalwe)

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
Wananchi wa kijiji cha Wami(mbalwe)
kilichopo katika kata ya Ihalimba wilaya ya Mufindi mkoani Iringa wameikataa
barabara inayotoka katika kijiji cha Vikula kwenda wami(mbalwe) kutokana na
kutengenezwa chini ya kiwango na kampuni ya Fabec civil,Building and Telecom
Engineers na kusababisha madhara ya kiafya kwa wananchi wa kijiji hicho.
 
Wakizungumza kwenye mkutano wa
hadhara ulihudhuriwa na mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa,walimwambia
mbunge huyu kuwa mkarasi aliyepewa kazi ya kutengeneza barabara hiyo ameahibu
ukilinganisha na ilivyokuwa hapo awali.
 
“Mheshimiwa Mbunge wetu Mahmoud
Mgimwa tunakuomba kweli hii barabara imetengenezwa chini ya kiwango kweli kweli
kiasi cha kusababisha magonjwa ya kifua na mafua na kusababisha kuanza kuingia
gharama ambazo zipo nje ya bajeti zetu sisi wananchi hivyo unapaswa kuliangalia
swali hili kwa njia ya kutuokoa wananchi wako” walisema wananchi
 
Wananchi hao waliongeza kwa
kusema kuwa mkandarasi huyo amekuwa anamajibu mabaya yasiyolizisha kwa wananchi
na viongozi wa kijiji hicho kwa kuwa kazi hiyo walipewa na serikali ya mkoa wa
Iringa hivyo mtu pekee wa kuwawajibisha ni serikali ya mkuu wa Mkoa na sio mtu
mwingine yeyeto yule.
 
“Mbunge huyu mkandarasi
anakiburi na anamajibu mabaya mno maana ametengeneza barabara chini ya kiwango
na kusababisha madhara kwa wananchi ila kila akiulizwa hatoe majibu ya
kurizisha kwa wananchi hata kwa viongozi wetu” alisema mmoja ya mwananchi  aliyekuwepo kwenye mkutano huo wa hadhara
 
Aidha wananchi hao walisema
kuwa utengenezwaji wa barabara hiyo unaotengenezwa na kampuni ya Fabec civil,Building
and Telecom Engineers umesababisha kukatika kwa masaliano ya kijiji hicho kwa
kuwa hakuna usafiri wa magari ya abiria yanayofanya safari kuelekea katika
kijiji hicho.
 
“Huku saizi hakuna usafiri wa
gari yeyeto  ya abiria ambao unafika huku
kutokana na mkandarasi huyu kukata mawasialiano ya barabara yetu hii ambayo
hapo awali ilikuwa inapitika vizuri na mabasi yalikuwa yanakuja  na tulikuwa tunasafiri saizi hakuna kitu
mheshimiwa mbunge Mgimwa” walisema wananchi
 
Akijibu hoja hizo za wananchi
wa kijiji cha wami(mbalwe) mbunge wa jimbo hilo Mahmoud Mgimwa alikiri kuwa
kuwa hata yeye hakubariani na utengenezaji wa barabara hiyo kutokana na
mkandarasi huyo kutengeneza barabara hiyo chini ya kiwango na kusababisha
madhara kwa wananchi wa kijiji cha wami(mbalwe)
 
“Saizi naona mnaguna hapa
kutokana na kupata ugonjwa wa mafua kutokana kutengenezabarabara chini ya
kiwango na kusababisha vumbi jingi ambalo linasababisha magonjwa hayo na
imekata mawasialiano ya usafiri kwa wananchi hao” alisema Mgimwa
 
Mgimwa alirazimika kumpigia
simu meneja wa TARURA wilaya ya Mufindi enjinia Sanga kusitisha malipo kwa
mkandarasi huyo kwa kuwa amekuwa akifanya kazi chini ya kiwango na amekuwa na
majibu ambayo siyo ya kulidhisha kwa wananchi pale wanapohoji kiwa njo na
kutengeneza barabara hiyo.
 
“Nakuomba meneja kuanzia sasa sitisha
malipo kwa mkandarasi huyo hadi pale atakapo kamilisha kutengeneza barabara
hiyo ili kurahisisha maendeleo kwa wananchi wa kijiji hicho” alisema Mgimwa
 
Kwa upande wake msimamizi wa
miradi ya kampuni ya Fabec civil,Building and Telecom Engineers Heri Rubeni
alisema kuwa magari na vitendea kazi vyao vingi vimeharibika toka wiki
iliyopita hivyo wapo kwenye matengenezo na vifaa hivyo vikikamilika ndio
watarudi kazini na kuanza kufanya kazi upya.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com