METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, July 30, 2019

SHAKA: Stiegler’s Gorge Ni Kielelezo cha Uhuru Wetu


“Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa Morogoro tunapongeza ujasiri wa Rais Dk John Magufuli kusimamia na kuzindua mradi wa Stiegler’s Gorge baada ya kucheleweshwa miaka mingi kukwamisha fursa za kiuchumi na sasa Tanzania ikithibitisha kwa vitendo kuwa ni nchi huru inayojiamulia mambo yake” Shaka


“CCM Mkoa Morogoro tunapongeza msimamo wa Serikali ya Dk Magufuli kwani baada ya kukamilika mradi huo, utakaotoa megawati 2,100 zitakazomaliza matatizo ya umeme na kusukuma mbele sekta za uvuvi, kilimo na utalii na hatimae milango ya fursa za ajira kwa vijana kufunguka” Shaka


“Stiegler’s Gorge ambao umekuwa ukipigwa vita na danadana nyingi toka kwa matapeli waliozowea kujipatia fedha na utajiri, utalipa heshima taifa kwa kujali na kusimamia maamuzi yake bila kutikiswa ambapo tumeonyesha namna gani kama taifa lililo huru hatuko tayari tena kukatishwa tamaa au kupangiwa, maendeleo, kupanga , kuchagua na kuamua lipi na kufanya na lipi la kuacha kwa maslahi ya taifa na watu wake” Shaka


“Mradi wa Stiegler’s Gorge utafungua fursa zilizojificha mkoani morogoro na nchi yetu . Utatupa heshima ya kusimamia mipango na maamuzi sahihi. Sis ni Taifa huru linalojali maendeleo . Hatuna umasikini bali wapo watu wachache waliokosa shime na ari ya uzalendo ” Shaka


“Nchi za kiafrika hazikupigania ukombozi ili zijitawale na kupangiwa mambo yake, badala yake zina wajibu wa kusimamia hatari ya umasikini kwa wananchi wake na kulinda heshima na kuonyesha ziko huru” Shaka


“Tumesimamia uamuzi huu ili kulinda utu na heshima ya kujitawala . Rais wetu kila kukicha anaumwa na umasikini uliopo . amedhamiria, amesimamia sasa anatekeleza, hiii ni ndoto iliosubiriwa miaka mingi na watanzania
baada ya kucheleweshwa kwa hakika kila mtanzania anayo kila sababu kusimama na Rais Magufuli ” Shaka


“Haiwezekani serikali ikahubiri mpango wa maendeleo bila kuwa na mkakati wa sera unaoonyesha kufikisha nishati ya umeme vijijini ambako ndiko kwenye mamilioni ya wakulima, wavivu na wafugaji wanaokosa umeme” Shaka


“Serikali ya awamu ya tano itatunza mazingira kwa kunusuru miti na misitu yetu isikatwe kuni na mkaa. Ili kuzuia tusiteketeze miti tuwe na umeme wa uhakika .Hiyo ndiyo tiba ya hakika .Umeme huchochea ujenzi wa viwanda kuelelea uchumi wa kati” Shaka


“Vijana kuweni na uzalendo na kulinda mradi huu katika kila hatua sambamba na kutumia fursa ya mradi huu kama chanzo kingine cha kuinua uchumi wa mtu moja moja kwa kufanya biashara za uzalishaji kwa vile kuna mahitajio makubwa kipindi hiki cha ujenzi na baada hivyo wanamorogoro waitumie vyema fursa hiyo” Shaka.


“Utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM unakwenda kwa kasi sana hapa Morogoro vijijini CCM iliahidi mambo kadhaa tunaendelea kuyatekeleza hatua kwa hatua hili ni moja wapo muelewe wananchi baada ya kukamilika mradi huu mkubwa wa kimkakati fursa zaidi za kiuchumi zitaongezeka ikiwemo kutunza mazingira, ujenzi wa viwanda, uwekezaji na uanzishaji miradi ya kiuchumi mikubwa na midogo kazi kwetu hususan vijana katika kutumia fursa hizi ” Shaka


Source @Majira@lajiji

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com