Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bi Rehema
Nchimbi,akimuapisha Rasmi Mkuu mpya wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida,
Bw Edward Mpogolo,aliyeteuliwa jana na Rais Dkt.Magufuli kuchukua nafasi
ya Miraji Mtaturu ambaye kachanguliwa kuwa Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki (CCM)
Mkuu Mpya wa wilaya ya Ikungi Bw.Edward
Mpogolo,akila kiapo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Singida,Bi.Rehema Nchimbi
wa pili kushoto ni Kaimu Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya
Viongozi wa Umma Kanda ya Kati,Dodoma Bi.Jasmin Bakari baada ya
kuapishwa rasmi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bi Rehema
Nchimbi,akimkabidhi barua Mkuu mpya wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida,
Bw Edward Mpogolo,aliyeteuliwa jana na Rais Dkt.Magufuli kuchukua nafasi
ya Miraji Mtaturu ambaye kachanguliwa kuwa Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki (CCM)mara baada ya kumuapisha rasmi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida,Bi.Rehema
Nchimbi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada
ya kumuapisha Mkuu Mpya wa wilaya ya Ikungi Bw.Edward Mpogolo,kulia ni
Kaimu Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda
ya Kati,Dodoma Bi.Jasmin Bakari baada ya kuapishwa rasmi.
Mkuu Mpya wa wilaya ya Ikungi Bw.Edward
Mpogolo,akizungumz na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya
kuapishwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Singida,Bi.Rehema Nchimbi .
Mkuu wa Mkoa wa Singida,Bi.Rehema
Nchimbi,akiteta jambo na Mkuu Mpya wa wilaya ya Ikungi Bw.Edward
Mpogolo,mara baada ya kumuapisha rasmi.
……………………..
Na.Alex Mathias,Singida
MKUU mpya wa Wilaya ya Ikungi Mkoani
Singida, Bw Edward Mpogolo ameapishwa leo rasmi kuanza majukumu yake
kama Mkuu wa Wilaya hiyo, kuchukua nafasi ya iliyoachwa wazi na Miraji
Mtaturu ambaye kwa sasa ni Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na
ikulu jana, uteuzi wa Bwana Mpogolo ulianza rasmi jana july 24, 2019,
kuwa mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.
Baada ya kuapishwa na Mkuu wa Mkoa wa
Singida, Bi Rehema Nchimbi, Mpologo ameahidi kushirikiana na uongozi wa
Halmashauri ya Wilaya katika kuhakikisha inakuwa na maendeleo sambamba
na kusimamia kikamilifu makusanyo ili kuinua uchumi wa eneo hilo.
“Ninamskuru Rais Dk,John Magufuli kwa
kuniteua,ninaahidi kuwa sitamwangusha ,nitahakikisha ninashirikiana na
Uongozi wa Mkoa na Halmashauri yangu ya Ikungi ili kuhakikisha tunafikia
malengo ya makusanyo katia Wilaya yetu”amesema Mpogolo.
Ameahidi kushirikiana na uongozi wa
halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ili kuhakikisha wanatumikia wananchi wa
Wilaya hiyo ikiwa wao ndio wawakilishi wa Rais katika eneo hilo.
Pia ameahidi kwenda kuisimamia Katiba ya
Nchi pamoja na Ilani ya Chama Tawala, Chama Cha Mapinduzi katika
kuwatumikia wananchi atakaowaongoza.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Sindida
Dk. Rehema Nchimbi amesema Mkuu wa Wilaya ndio msimamizi mkuu wa Kamati
ya ulinzi na usalama na ndio msimamizi mkuu wa shughuli za maendeleo
katika eneo husika na kumtaka kwenda kusimamia vyema miradi ya Serikali
inayotekelezwa Wilayani humo.
“Mkuu wa Wilaya yeye ni msimamizi mkuu na
muwakilishi wa Rais katika Wilaya na ndio mkuu wa kamati ya ulinzi na
usalama na ukasimamie miradi yote inayotekelezwa Wilayani humo” amesema
Dtk Rehema.
Hata hivyo amemwambia kuwa Wilaya ya
Ikungi inamiradi mbalimbali ya maendeleo iliyokusudiwa kwenye malengo
ikiwemo miradi ya visima 28 vilivyokusudiwa kukamilishwa .
Aidha Dk.Nchimbi amesema upande wa Singida magharibi wanamiradi ya visima 13 na Singida mashariki visima 15 .
Amebanisha malengo mengine yaliyowekwa
kwa Wilaya hiyo kuwa ni kilimo cha zao la michikichi ekari 200 pamoja na
kilimo cha zao la korosho.
0 comments:
Post a Comment