METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, July 26, 2019

Mchakato wa Tathmini Mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga Katika Uchumi Waiva

Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Sekta kuu ya Uchukuzi, Mhandisi. Aron Kisaka akizungumza wakati wa kikao cha kujadiliana hatua zilizofikiwa katika mchakato wa kuanza matumizi ya mfumo wa kutathmini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika ukuaji wa uchumi nchini. Kutoka kushoto ni Mtakwimu Mkuu wa Serikali toka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ua Usafiri wa Angaa (TCAA), Hamza Johari.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Hamza Johari. akizungumza wakati wa kikao cha kujadiliana hatua zilizofikiwa katika mchakato wa kuanza matumizi ya mfumo wa kutathmini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika ukuaji wa uchumi wa Taifa leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mtakwimu Mkuu wa Serikali toka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Sekta kuu ya Uchukuzi, Mhandisi. Aron Kisaka na Mtakwimu Mkuu, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar, Mayasa Mahfoudh Mwinyi.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya kubaini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika uchumi wa Taifa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi(hayupo pichani) alipokuwa akifungua kikao cha kujadiliana hatua zilizofikiwa kabla ya kuanza matumizi ya mfumo wa kutathmini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika ukuaji wa uchumi wa Taifa leo jijini Dodoma.
Katibu wa Kamati ya Kubaini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika Uchumi wa Taifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Udhibiti Uchumu toka Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Danieli Malanga akiwasilisha taarifa fupi ya hatua zilizofikiwa katika mchakato wa kuelekea kuanza matumizi ya mfumo rasmi wa tathmini ya mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika uchumi wa Taifa wakati wa kikao cha kamati hiyo leo jijini Dodoma.
Katibu wa Kamati ya Kubaini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi toka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Daniel Masolwa akichangia hoja wakati wa kikao cha kujadili hatua zilizofikiwa katika mchakato wa kuelekea kuanza matumizi ya mfumo rasmi wa tathmini ya mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika uchumi wa Taifa wakati wa kikao cha kamati hiyo leo jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mwenza wa Kamati ya Kubaini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika Uchumi wa Taifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Udhibiti Uchumu toka Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Danieli Malanga
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta Kuu ya Uchukuzi), Mhandisi. Aron Kisaka (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Kubaini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika Uchumi wa Taifa wakati wa kikao cha kujadiliana hatua zilizofikiwa katika mchakato wa kuanza matumizi ya mfumo wa kutathmini mchango wa Sekta ya Usafiri wa Anga katika ukuaji wa uchumi nchini. (Picha na: Idara ya Habari MAELEZO)
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com