METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, July 23, 2019

JESHI LA POLISI DODOMA LANASA MTU MMOJA ALIYETAPELI KWA KUJIFANYA POLISI

***************
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Jeshi la polisi mkoani Dodoma limemshikilia RAJAB RAMADHAN[32] aliejifanya askari polisi Kwa kutapeli watu mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake jijini Dodoma Leo Julai 23,2019 Kamanda wa polisi mkoani hapa Gilles Muroto amesema kwa muda Mrefu kijana huyo anayeishi eneo la Area A Mjini Dodoma amekuwa akijipatia huduma mbalimbali kwa udanganyifu akijifsnya askari polisi na kutishia watu kwa silaha bandia.
Kamanda Muroto ametaja vifaa alivyokuwa navyo mhalifu huyo kuwa ni sare ya polisi Jangle Green,pistol ya bandia na hoster yake,picha akiwa na sare za jeshi [JWTZ] huku uchunguzi wa awali ukionesha kuwa kijana huyo alishawahi kuhudhuria mafunzo ya JKT na Kufukuzwa kwa utovu wa nidhamu.
Katika hatua nyingine Kamanda Muroto amesema jeshi hilo limekamata vifaa vya NIDA ambavyo ni kamera 12 ambapo mtumishi wa NIDA Ezekiel Subugo [24] aliiba vifaa hivyo ofisini na kuwauzia watu mitaani na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.
Hata hivyo,Jeshi hilo limemkamata Musa Pungu akiwa na madawa ya kulevya aina ya Heroin kiasi cha kete 132 zilizofungashwa katika vinailoni ambapo Kamanda Muroto amesema kijana Musa ameharibu vijana wengi kwa madawa ya kulevya katika Mtaa wa Hazina jijini Dodoma hivyo mtuhumiwa na wenzake wanne watafikishwa mahakamani.
Kamanda Muroto ametoa wito kwa jamii kujihadhari na Matapeli katika jiji la Dodoma na hakuna Fedha zinazokuja kiurahisi bila kufanya kazi halali.
Sanjari na hayo,Kamanda Muroto ameipongeza Kampuni ya INNOMAX kwa kulikabidhi jeshi hilo pikipiki mbili mpya aina ya HAOJUE na HONGLOG zenye thamani ya zaidi ya Tsh.Milioni 4 Kwa ajili ya kufanyia doria huku akiwaasa Watanzania wengine kuwa na uzalendo wa kusaidia jeshi hilo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com