Bondia
Muingereza Anthony Joshua akiwa chini baada ya kuangushwa na mpinzani
wake, Mmarekani mwenye asili ya Mexico, Andy Ruiz Jr Alfajiri ya leo
ukumbi Madison Square Garden mjini New York kwenye pambano la uzito wa
juu. Joshua amevuliwa ubingwa wa dunia wa uzito wa juu duniani baada ya
kupigwa kwa Technical Knockout (TKO) raundi ya saba. Ruiz hajawahi
kuangushwa kabla, lakini naye leo alikalishwa chini raundi ya tatu,
kabla ya kuinuka na kuendelea. Joshua mwenye urefu wa futi sita atajaribu kurejesha mataji yake ya IBF, WBA na WBO katika pambano la marudiano Novemba. Hilo
ni pambano la kwanza Joshua kupoteza baada ya kushinda mapambano yake
yote 22 ya awali, 21 kwa knockout, wakati Ruiz mwenye urefu wa futi nne
ameshinda pambalo la 32 na 22 kwa KO, huku akiwa amepoteza pambano moja
piaPICHA ZAIDI SOMA HAPA
0 comments:
Post a Comment