Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti Dkt Christine Ishengoma, ikikagua kitalu nyumba cha kuzalisha mbegu bora za viazi vitamu mara baada ya kutembelea Taasisi ya utafiti wa Kilimo-TARI Kibaha juzi tarehe 22 Machi 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti Dkt Christine Ishengoma, ikikagua kitalu nyumba cha kuangalia na kuthamini magonjwa ya migomba yanayosababishwa na minyoo mara baada ya kutembelea Taasisi ya utafiti wa Kilimo-TARI Kibaha juzi tarehe 22 Machi 2019.
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti Dkt Christine Ishengoma, ikikagua maabara ya kusafisha na kuboresha mbegu safi mara baada ya kutembelea Taasisi ya utafiti wa Kilimo-TARI Kibaha juzi tarehe 22 Machi 2019.
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti Dkt Christine Ishengoma, ilipotembelea shamba la mihogo mara baada ya kutembelea Taasisi ya utafiti wa Kilimo-TARI Kibaha juzi tarehe 22 Machi 2019.
Na Mathias
Canal-Wizara ya Kilimo, Pwani
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na
Maji imeipongeza Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kwa kufanya
tafiti zenye tija na zinazolenga kumbadilisha mkulima wa kawaida ili aweze
kupiga hatua kimaendeleo katika kilimo na maisha yake kwa ujumla.
Kamati hiyo imesema kuwa ili kuwezesha wakulima
na wafanyabiashara wa Tanzania kuchangamkia fursa ya kilimo cha muhogo, kwani Mei,
2018 ulisainiwa mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya China
kuruhusu bidhaa za muhogo mkavu kutoka Tanzania kuingia katika soko la China.
Akizungumza juzi tarehe 22 Machi 2019 mbele ya
watumishi wa kituo cha utafiti TARI kilichopo Kibaha Mkoani Pwani Mwenyekiti wa
kamati hiyo Mhe Dkt Christine Ishengoma amekipongeza kituo hicho kilicho chini
ya Wizara ya Kilimo huku akizitaka Taasisi zote za utafiti nchini kutangaza
kazi wanazozifanya.
“Kamati inazitaka Taasisi zote za utafiti wa
kilimo nchini kuhakikisha kuwa inatangaza kwenye vyombo vya habari na
kwingineko tafiti zao zote ili kulinda kazi kubwa na nzuri wanazozifanya maana
kukaa kimya kunafifisha juhudi za kazi zao” Alisisitiza
Dkt Ishengoma alitoa wito kwa Watanzania kuchangamkia
fursa ya kilimo hususani kilimo cha muhogo ambacho kimeonesha kuwa na tija
kubwa, pia amevitaka vituo vya utafiti wa kilimo viwawezeshe wakulima kupata
mbegu bora na mbinu za kisasa ili waongeze uzalishaji na kukidhi mahitaji ya
soko hilo.
Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo
ameihakikishia Wizara ya kilimo kuwa itapitisha Bajeti yote inayohusisha maswala
ya utafiti ili kuongeza tija na ufanisi katika kazi ya utafiti.
Alisema sio jambo jepesi kuendeleza kilimo pasina
kuwa na tafiti bora hivyo kamati inatambua umuhimu wa utafiti nchini na kwa
maana hiyo imeridhia kushirikiana na taasisi hizo za utafiti ili kuwanufaisha
wakulima.
Kwa
upande wake Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amekiri sekta ya kilimo
haiwezi kuendelea bila kufanya utafiti kuanzia ngazi ya awali ya kilimo kwa
kufanyika utafiti wa udongo, mbegu, Mbolea na viuatilifu.
Alisema
kuwa Wizara ya kilimo ina mpango wa kupeleka maazimio ya kuwa na sharia ya
kulinda tafiti mbalimbali zinazogunduliwa nchini.
Kadhalika,
Waziri Hasunga ameungana na kamati hiyo kuitaka TARI kutangaza kazi zake
inazozigundua ili zifahamike kuliko kuzifungia ofisini.
Vilevile
amewataka watafiti katika vituo vyote vya utafiti kuhakikisha kuwa wanafanya
kazi kwa umoja, kutokuwa wabinafsi na kushirikishana kazi zao kwani kufanya
kazi kwa ubinafsi kunarudisha nyuma juhudi za maendeleo ya Kilimo.
Mhe
Hasunga alisema kuwa “Umefika wakati kila utafiti unaofanywa na wagunduzi wetu
uwe una haki miliki kwamba haki ya kazi ya mtaalamu ijulikane na muhusika
atambulike ili kusiwe na mtu mwingine wa kuiba tafiti isiyomuhusu”
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment