METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, January 24, 2019

WAKAZI WA VINGUNGUTI WAJITOKEZA KWA WINGI KATIKA MDAHARO WA KUPINGA RUSHWA YA NGONO ULIOANDALIWA NA POLISI DAWATI LA JINSIA ILALA


Kesi nyingi zinazoripotiwa kwa sasa katika madawati ya jinsia na watoto zimebainisha kuwa watu wengi wamekuwa wakijifanyia ukatili pasipo wenyewe kujijua.

Hayo yameelezwa mapema jana jijini Dar es salaam na Afande Christina Onyango ambaye ni Mratibu wa Dawati la jinsia na watoto Mkoa wa Kipolisi  Ilala katika muendelezo wa kampeni ya kupinga rushwa ya ngono katika mkoa huo.

Afande huyo alisema watu wengi wamekuwa wakitoa rushwa ya ngono bila kujua kuwa wanalolifanya ni kosa kisheria kwa mtendaji na hata mtendewa Kwa kuwa inahesabiwa ni rushwa kama rushwa nyingine.

Aliongezea kuwa kitendo hicho kinaleta madhara makubwa katika jamii ikiwemo kushusha hadhi ya mtu, kufanya kazi kwa woga na hata kusababisha kupata magonjwa ya zinaa kama gono na ukimwi.

Aliendelea kusema kuwa program hiyo ilianza rasmi kwenye siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia na mpaka sasa haina mfadili wa kudumu ila kwa hii ya leo imefadhiliwa na Women Fund kwa kushirikiana na Dawati ya jinsia na watoto mkoa wa Kipolisi Ilala.

Katika Mdaharo huo uliofanyika katika kata ya Vingunguti jijini Dar es salaam huku Mgeni Rasmi akiwa ni Adam Maru ambaye ni OCD wa Buguruni , wamesema kuwa lengo ni kuzifikia kata zote za Mkoa wa Kipolisi Ilala ili wananchi wafahamu madhara ya rushwa ya ngono ndani ya jamii yao.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Buguruni OCD Adam Maru alisema kesi nyingi wanazozipokea ni za ukatili wa majumbani hasa kwa watoto, wanawake lakini pia hata wanandoa kufanyiana ukatili wenyewe kwa wenyewe.

Aliongeza kuwa kesi hizi kwa sasa zimepungua na hii ni kutokana na kuwepo kwa elimu kubwa inayotolewa pamoja na uwepo wa madawati katika vituo vya polisi, kwa kuwa hapo mwanzo watu walikuwa wakibaki na machungu yao moyoni bila kufahamu wapi ni mahali sahii pa kuyapeleka.

Aidha Kamanda  Adam amewataka wananchi kuweza kuvunja ukimya na kuamua kufunguka juu ya ukatili wa kijinsia na kuacha tabia ya kuficha mambo kwa kuhofia mtendaji wa ukatili hata akiwa ni ndugu wa karibu aidha mjomba, kaka hata baba mdogo na kuamua kumripoti katika dawati la Jinsia.
Kikundi cha Milembe Joging kikiwasili katika viwanja vya Vingunguti Machinjioni mapema jana jijini Dar es salaam, katika Mdaharo wa kupinga Rushwa ya Ngono.
Afande Christina Onyango ambaye ni Mratibu wa Dawati la jinsia na watoto Mkoa wa Kipolisi  Ilala akiongea na wakazi wa vingunguti katika Mdaharo ulioandaliwa na Dawati la jinsia mkoa huo.

Inspekta Lydia kutoka Dawati la jinsia Chanika akimkaribisha Mgeni Rasmi ambaye ni Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Buguruni.

Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Buguruni OCD Adam Maru akiongea na wakazi wa kata ya vingunguti juu ya changamoto ya Rushwa ya Ngono hapa nchini.

Naibu Meya wa Ilala ambaye pia ni Diwani wa Vingunguti Bw. Omary Kumbilamoto akiwasalimia wakazi wa kata hiyo.

Meza kuu ikiwa katika majadiliano.
Wakazi wa Vingunguti na maeneo ya karibu wakifuatilia Mdaharo ulioandaliwa na Dawati la Jinsia mkoa wa Kipolisi Ilala.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com