METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, January 6, 2019

Mbunge Nyamagana akagua miradi mbalimbali ya maendeleo “vyoo vinatisha”

Mbunge Jimbo la Nyamaganamkoani Mwanza, Stanslaus Mabula (CCM) ameendelea na ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo hilo ikiwemo elimu, afya, maji na barabara kusaidia ukamilishaji wa miradi hiyo kupitia fedha za mfuko wa jimbo.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Ziara ya mbunge Stanslaus Mabula pia ilifika katika Shule ya Msingi Amani Kata ya Butimba na kujionea hali tete ya vyoo na kuchangia ukarabati wake.
Mbunge Stanslaus Mabula alifika katika Shule ya Msingi Amani iliyopo Kata ya Butimba na kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha jengo hili kwa ajili ya kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa.
Mbunge Stanslaus Mabula pia aliwasili katika Shule ya Msingi Igoma C na kusaidia ukarabati wa shule hiyo.
Ukarabati ukiendelea katika Shule ya Msingi Igoma C Jijini Mwanza.
Ukarabatai katika Shule ya Msingi Igoma C.
Mbunge Stanslaus Mabula pia alisaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi Kata ya Kishiri.
Kituo cha Polisi Kata ya Kishiri Jijini Mwanza.
Mbunge Stanslaus Mabula pia alisaidia ujenzi wa Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Mahina Kati Kata ya Mahina inayojengwa kwa nguvu za wananchi.
Mbunge Stanslaus Mabula akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali katika Kata ya Mahina.
Tazama BMG Online TV hapa chini
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com