Naibu
Waziri wa Madini, Doto Biteko (katika) akikagua mgodi wa MMC wa dhahabu uliopo
Wilayani Mvomero mkoani Morogoro jana tarehe 9 Desemba, 2018.
Mwakilishi wa Mgodi wa MMC upande wa uzalishaji (wa kwanza kulia), akimwelekeza jambo Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (katikati) wakati alipokuwa akikagua mgodi huo alipokuwa katika ziara yake ya ukaguzi wa migodi ya dhahabu Mkoani Morogoro hapo jana tarehe 9 Decemba, 2018.
Wananchi
wa Vijiji vya Mtukule na Mangae wakimsikiliza Naibu Waziri wa madini, Doto Biteko
jana tarehe 9 Disemba, 2018 Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro.
Muonekano wa Mgodi wa MMC uliopo wilayani Mvomero mkoani Morogoro.
v Wachimbaji
wadogo nchini kote mnapoingia mikataba lazima Serikali itabue mikataba hiyo.
Naibu
Waziri wa Madini Doto Biteko ameutaka Mgodi wa MMC kulipa fidia kwa wananchi wa
vijiji vya Mtukule na Mangae ambao walipisha mgodi huo lakini hawakuwahi
kulipwa fidia yao.
Naibu
Waziri Madini Doto Biteko ametoa maagizo hayo jana tarehe 9 Desemba, 2018
alipotembelea Mgodi wa MMC lengo likiwa ni kukagua shughuli zilizokuwa
zikiendelea za uchimbaji pamoja na kuwa waliagizwa kusimama kufanya shughuli
hizo hadi watakapo lipa fidia kwa wananchi hao wanaodai haki yao.
Biteko
ameeleza kuwa tangu Mgodi huu kuanza umekuwa ukiendelea na shughuli zake za
uchimbaji lakini wananchi waliouzingira mgodi huu hawajelipwa haki yao, lepeni
fidia kwanza alafu kama uwekezaji wenu ni halali mtaendelea.
“MMC
hakikishani kuwa wananchi wote wanalipwa haki yao na sio laki tano niliyoambiwa
kuwa wamelipwa,” alisema Biteko.
Aidha,
Biteko amemwagiza Mkuu wa Wilaya wa Mvomero, Mwalimu Mohamed Utally kuhakikishe
kuwa, wananchi wote wanachambuliwa ili kujua mwenye haki ya kulipwa na kama
ardhi ni ya kijiji ijulikane ni kiasi gani ili kila mmoja wao alipwe haki yao,
ili kama uwekezaji ni wa haki wananchi wapishe uwekezaji huo.
Biteko
aliendelea kueleza kuwa maendelea hayawezi kupatikana kama mgodi na wananchi
hawako vizuri, lazima wawekezaji wapitia hatua mbalimbali kama vile ya
kujitambulisha kwa Serikali ya Kijiji hadi ya Wilaya.
“Na
ili Mgodi huu uwe na adhabu lazima shughuli zake za uchimbaji zisimame hadi
hapo watakapokuwa wamelipa wananchi fidia yao, alisema Naibu Madini Biteko.
Akizungumza
katika hadha hiyo, Biteko alisema kuwa wananchi pia wamepeta adha ya barabara,
na wamelazimishwa kupita barabara nyingine ambayo hairidhishi.
Nakwagiza
Mkuu wa wilaya na hili pia ulifanyie kazi kwa kushirikiana na Mkuu wa TARURA
mkoa ili wananchi hawa wapate haki yao.
“Tunataka
tuondoe ubabaishaji na uongouongo kwenye Sekta ya Madini,” alisema Biteko.
Pia,
Naibu Waziri wa Madini Biteko ametoa wito kwa Watanzania wote hasa Wachimbaji
wadogo kuhakikishe kuwa, kila wanapoingia mikataba na Wawekezaji wageni lazima
Serikali itambue mikataba hiyo.
Biteko
aliongeza kuwa, lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha kuwa watanzania
hawanyonywi na vile vile wawekezaji hawaingii mikataba ambayo sio sahihi alafu
baadaye wanalaumu serikali ya Tanzania kuwa inanyanyasa wawekazaji.
Aliongeza
kuwa sisi Watanzania tusiwaingize wawekezaji mkenge alafu nchi ya Tanzania
inaonekane kuwa inawanyanyasa wawekezaji, futeni sharia zilizopo.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mwalimu Mohamed Utally alihaidi kuwa
atayafanyia kazi maagizo haya na atasimamia kuhakikisha kuwa kila mwananchi
analipwa haki yake.
0 comments:
Post a Comment