Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani leo tarehe 12 Novemba, 2018 amevunja rasmi Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) iliyokuwa ikiongozwa na Dkt. Gideona Kaunda.
Uamuzi huo ameutoa katika Mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati jijini Dodoma.
Alisema kuwa, Bodi hiyo iliundwa mwaka 2017, kwa mujibu wa Sheria ya Wakala Vijijini Na.8 ya Mwaka 2005 (The Rural Energy Act. No.8 of 2005).
“ Bodi hii imetekeleza majukumu yake kwa takriban mwaka mmoja (1) sasa na katika kipindi hicho ambapo Bodi hii imekuwepo, ninapenda kuwajulisha kwamba kwa ujumla sijaridhishwa na utendaji wake,” alisema Dkt Kalemani.
Hivyo alieleza kuwa, kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu 9(3)(b) cha Sheria Na. 8 ya Nishati Vijijini ya 2005, ameamua kuivunja Bodi hiyo kwa kutengua uteuzi wa Mwenyekiti pamoja na Wajumbe wa Bodi.
Aliongeza kuwa, Bodi nyingine mpya itaundwa baadaye kwa mujibu wa Sheria ya Nishati Vijijini ya mwaka 2005. Bodi hiyo ilizinduliwa mwezi Aprili mwaka 2017 na ina wajumbe Saba.
Monday, November 12, 2018
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Anna Joram Gidarya, amewataka wananchi wa Wilaya ya Busega kutoa maoni kwa uhuru kuhusu ombi la k...
-
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Laigwnani Metui Ole Shaudo mapendekezo ya Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro kuhusu namna bor...
-
*AWASIHI WANASIASA KUJIKITA KATIKA SIASA SAFI NA UONGOZI BORA *WASITUMIE UONGO NA SHIDA ZA WATU KUSAKA UMAARUFU WA KISIASA ...
-
Waziri wa kilimo Mhe Japhet Ngailonga Hasunga (Mb) Naibu Waziri wa Wizara ya kilimo Mhe Innocent Lugha Bashungwa Na Mathias C...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment