Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, WK)
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakimsikiliza kwa makini waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018.
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakimsikiliza kwa makini waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018.
Na Mathias Canal-WK,
Mtwara
Wakulima wa zao la korosho wa Wilaya ya Tandahimba na Masasi wamekubali
kuuza korosho zao mbele ya Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) kutokana
na kuridhia na kukubaliana na maamuzi ya serikali.
Hayo yamejili katika mnada wa nne wa msimu wa uuzaji korosho
2018/2019 uliojumuisha kampuni za ununuzi 11 katika maghala tofauti uliofanyika
katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika
kijiji na kata ya Mdimba, Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba alisema
kuwa bei ya zao la korosho imeonyesha mwelekeo wa kushuka katika mwaka
2018/2019 tofauti na hali ilivyokuwa katika msimu wa mwaka 2017/2018 ambapo bei
ya zao hilo ilifikia shilindi 4,128
Katika mkutano huo wakulima wa korosho walikubali mbele ya
waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Tizeba kuanza kuuza korosho zao kwa bei ya juu ya
shilingi 3,016 huku bei ya chini ikiwa ni shilingi 3000.
“Wafanyabiashara wasipangiwe muda wa kuchukua korosho ghalani
kwa ajili ya usafirishaji na wasipangiwe kutumia bandari gani, wawe huru
kulingana na maagizo yaliyotolewa na Rais Magufuli’’
“Nitashangaa sana kuona mnunuzi mwenye akili timamu akitoa
barua na kutaka kuuziwa korosho chini ya shilingi 3,000 au akitaka kwa shilingi
2,500” Alikaririwa Dkt Tizeba
Kufuatia hali hiyo tarehe 26 Octoba 2018 Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa alitangaza maamuzi ya
serikali kusimamisha minada yote hadi suala hilo litakapopatiwa ufumbuzi.
Kufuatia uamuzi huo tarehe 28 Octoba 2018 Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli alikutano na wanunuzi wa zao la
korosho katika mkutano uliokuwa ukiendelea kati ya wanunuzi hao na Waziri Mkuu na
kutoa msimamo wa serikali kuhusu zao hilo kufuatia kuwepo kwa mvutano wa bei ya
zao hilo kati ya wanunuzi na wakulima.
Katika mnada huo wa nne uliohudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa
Mtwara Mhe Gelasius Gasper Byakanwa, Waziri wa kilimo Dkt Tizeba alisema kuwa matokeo
ya mnada huo hayakuwa mabaya ukilinganisha na minada iliyopita katika msimu huu
wa 2018/2019 ambapo bei ilishuka.
Alisema baada ya Rais Magufuli kutangaza msimamo wa serikali
kuwa bei ya kiwango cha chini ya mnadani katika msimu wa 2018/2019 kuwa
shilingi 3000 kwa kilo moja ya korosho, wafanyabiashara wameitikia wito kwa
kuweka bei nzuri mnadani.
Aidha, Waziri wa kilimo alisema kuwa katika vikao vingi vya
serikali vilivyotuama kujadili mwenendo wa zao hilo kwa mujibu wa kifungu cha 8
cha sheria ya Tasnia ya Korosho Na 18 ya mwaka 2018 ameielekeza Bodi ya korosho
kupata kibali cha waziri wa kilimo na waziri mkuu kabla ya kuyafanyia maamuzi.
Alisisitiza kuwa mnunuzi akishalipa ushuru katika Halmashauri
moja hapaswi kudaiwa kulipa ushuru huo katika Halmashauri nyingine, Bodi
kutotoa bei elekezi, Tozo ya Bodi ya korosho ambayo iliongezwa kwa msimu wa
mwaka 2018/2019 kufikia shilingi 17 kwa kilo irudi shilingi 10 kwa kilo kama
ilivyotozwa msimu wa 2017/2018
Wanunuzi wa korosho wana hiari ya kusafirisha korosho kwenda
nje ya nchi kupitia bandari ya mtwara, Dar es salaam au Tanga huku wanunuzi
wakiruhusiwa kwenda na magunia yao kununua korosho ya wakulima, Bodi ya korosho
kuangalia utaratibu wa wabanguaji wadogo kupata/kununua korosho katika mfumo wa
mnada, sambamba na dhamana ya mnada (Bill Security) kupungua.
Dkt Tizeba alisema kuwa baada ya maelekezo ya serikali kuhusu
mwenendo wa zao la Korosho katika hatua ya kwanza ya utekelezaji Wizara yake
ilianza kutathmini kuhusu mfumo mzima wa uuzaji wa korosho hatimaye kufikia
uamuzi huo.
Aliwasisitiza wakulima kutokata tamaa na minada kwani ni
kawaida kwa bei za mazao kupanda na kushuka kulingana na uzalishaji katika nchi
zingine pamoja na soko la Dunia.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment