METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, October 29, 2018

Vijiji vitatu vyapata umeme Chato


Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani akizindua huduma ya umeme katika Kijiji cha Bupandwampuli wilayani Chato mkoani Geita.
 Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani akizindua huduma ya umeme katika Kijiji cha Butarama   wilayani Chato mkoani Geita.


Moja ya nyumba iliyounganishwa na huduma ya umeme katika Kijiji cha Butarama wilayani Chato mkoani Geita.
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kikumbaitale wilayani Chato kabla ya kuzindua huduma ya umeme katika Kijiji hicho.

Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani amefanya ziara wilayani Chato mkoani Geita ya kukagua mradi wa usambazaji umeme vijijini wa Awamu ya Tatu ( REA III).

Akiwa wilayani humo amezindua huduma ya umeme katika Kijiji cha Bupandwampuli, Kikumbaitale na Butarama.

Vijiji 74 wilayani Chato vipo katika mpango wa kupelekewa umeme kupitia REA III ambapo mpaka kufikia tarehe 27 Oktoba, 2018,   Vijiji 20 vimeunganishwa na huduma hiyo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com