Waziri
wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe akisoma kijarida
cha Hifadhi ya Taifa ya Saaadani alipotembelea banda la maonesho la Hifadhi
hiyo katika Tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Oktoba
20,2018. Kulia ni Mhifadhi Utalii wa Saadani Bi. Apaikunda Mungure.
Hifadhi
ya Taifa ya Saadani kupitia Tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo
limetangaza ofa Watanzania na wasio Watanzania kutembelea hifadhi hiyo kuanzia
Oktoba 25, 26 na 27 mwaka huu kujionea vivutio mbalimbali vya Utalii.
Akizungumza
Mhifadhi Utalii, Hifadhi ya Saadani, Bi. Apaikunda Mungure amesema ofa hiyo ni
maalum kwa msimu huu wa tamasha la Sanaa Bagamoyo ambapo kwa kiasi cha
Tsh. 91,000 ni gharama kwa Raia wa Tanzania pamoja na Afrika
Mashariki huku wageni kutoka nje ya Afrika Mashariki hao watalipia US$120 tu.
“Ofa
hii itanda kwa muda wa siku tatu. Oktoba 25, 26 na 27. Wageni
wataenda Saadani na kurudi hapa Bagamoyo. Kwa kiasi hicho cha Tsh. 91,000
inajumlisha usafiri wa magari ya Kitalii, usafiri wa kuzunguka na boti kwenye
makutano ya Mto Wami na bahari ya Hindi.
Pia
watapata kifungua kinywa, chakula cha mchana na vinywaji na kutembelezwa kwa
safari za kuangalia wanyama na magari” alieleza Bi. Apaikunda
Mungure.
Ameongeza
kuwa kwa familia itakayokuwa na motto atamlipia Tsh. 71,000.
Saadani ni
hifadhi ya kipekee ambapo Nyika na bahari vinakutana pamoja. Ndani
ya hifadhi hiyo ina aina mbalimbali za wanyama pori, fukwe ya bahari ya hindi.
Iko
katika mkoa wa Pwani na Tanga
Watanzania
ambao wapo Bagamoyo na miji jirani ya Dar es Salaam ni fursa ya kujitokeza
kwenda kujionea Utalii wa ndani wenye kila aina ya vivutio vya Wanyama na
safari zitakuwa kila siku kwa wageni kuanzia saba ambao wao kila mmoja atakaa
kwa siti tena dirishani (window seat).
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment