Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akisisitiza
jambo wakati akizungumza kwenye Jubilee ya miaka 50 ya shule ya Sekondari
Buluba iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga juzi tarehe 25 Octoba 2018. (Picha
Zote Na Mathias Canal, WK)
Waziri wa kilimo
Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada
ya kuwasili eneo la shule ya sekondari Buluba kwa ajili ya kushiriki Jubilee ya
miaka 50 ya shule hiyo iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga, juzi tarehe
25 Octoba 2018.
Waziri wa
kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akisisitiza jambo wakati akizungumza
kwenye Jubilee ya miaka 50 ya shule ya Sekondari Buluba iliyopo katika Manispaa
ya Shinyanga juzi tarehe 25 Octoba 2018.
Na Mathias
Canal, WK-Shinyanga
Waziri wa
kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) amefanikisha upatikanaji wa kiasi cha
shilingi Milioni 63,975,800 kwa ajili ya uendelezaji wa miundombinu mbalimbali
ya shule ya sekondari Buluba iliyopo Shinyanga Mjini inayomilikiwa na Chama
Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Shinyanga (SHIRECU).
Kiasi hicho
cha fedha kimepatikana wakati wa harambee aliyoiendesha tarehe 25 Octoba 2018
wakati wa Jubilee ya miaka 50 ya shule hiyo ambapo awali ilitanguliwa na
mahafali ya 48.
Katika
harambee hiyo fedha taslimu kiasi cha shilingi Mil 17,448,000 zilipatikana,
Ahadi zilizotolewa ni Mil 20,365,800 huku vifaa vilivyochangwa ni Nondo moja
pamoja na mifuko 1307 ya saruji vyenye jumla ya shilingi Mil 26,162,800
Fedha hizo
pamoja na vifaa vya ujenzi vitatumika kutatua changamoto za shule hiyo ambazo
ni pamoja na kukabiliana na upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi, Upungufu
wa vitabu vya kujifunzia darasani, uhaba wa vyoo, sambamba na ujenzi wa uzio.
Vilevile
utatuzi wa changamoto ya vifaa vya ufundishaji kama kompyuta, kuboresha maktaba
pamoja na upatikanaji wa vitabu vya kutosha.
Awali,
akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza katika hafka hiyo ya Jubilee ya
miaka 50, Waziri Tizeba alimuagiza Mrajisi wa vyama vya Ushirika Ndg Tito Haule
kufuatilia taarifa za mapato na matumizi ya shule hiyo haraka iwezekanavyo.
"
Wakati tunachangia fedha hizi kwa ajili ya shule na mimi kwa dhamana niliyonayo
ninamuagiza Mrajisi wa vyama vya ushirika aje apate ripoti ya fedha ya hii
shule kwa sababu hii shule ni mali ya umma" Alisisitiza Dkt Tizeba
Alisema
kuwa serikali imechoka kusikia Ushirika ni sawa na wizi hivyo imeweka juhudi za
makusudi za kuwabaini wabadhilifu wa mali za Ushirika na kuwachukulia hatua
kali za kisheria.
"Tunataka
tusikie Ushirika ni sawa sawa na Maendeleo ya wakulima au wana Ushirika
wenyewe" Alisema
Katika
Jubilee hiyo ya Shule ya sekondari Buluba iliyoanzishwa mwaka
1967, Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) alikuwa mgeni
rasmi akimuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim
Majaliwa (Mb).
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment