METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, October 21, 2018

DKT TIZEBA ACHANGIA MIFUKO 100 YA SARUJI, MABATI NA MIL 1 UJENZI WA ZAHANATI JIMBONI BUCHOSA

Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza Mhandisi Dkt Charles Tizeba akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji na kata ya Bukyaheke akiwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza kukagua shughuli za utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka 2015, jumapili tarehe 21 Octoba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, WK)
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza Mhandisi Dkt Charles Tizeba akikagua ujenzi wa soko la kisasa la samaki wakati akiwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza kukagua shughuli za utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka 2015, jumapili tarehe 21 Octoba 2018. 
Sehemu ya wananchi wa kijiji na kata ya Bukyaheke wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza Mhandisi Dkt Charles Tizeba akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wakati akiwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza kukagua shughuli za utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka 2015, jumapili tarehe 21 Octoba 2018. 
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza Mhandisi Dkt Charles Tizeba akikagua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Bukyaheke wakati akiwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza kukagua shughuli za utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka 2015, jumapili tarehe 21 Octoba 2018. 

Na Mathias Canal, Bulyaheke-Mwanza

Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza Mhandisi Dkt Charles Tizeba jumapili tarehe 21 Octoba 2018 alifanya ziara ya siku moja ya kikazi katika jimbo la Buchosa Mkoani Mwanza kukagua shughuli za utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

Pamoja na mambo mengine katika ziara hiyo Dkt Tizeba alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wananchi kwa kuendelea kuiamini serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli.

Pongezi hizo pia zinatuama kuwashukuru wananchi kwa kukiamini Chama Cha Mapinduzi kwa kumchagua Rais, Mbunge na madiwani wanaotokana na CCM.

Akihutubia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Bukyaheke Dkt Tizeba amechangia jumla ya shilingi Milioni moja kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho sambamba na kuchangia mifuko 100 ya saruji.

Vilevile, Mbunge huyo amewataka wananchi kushiriki katika shughuli za ujenzi wa zahanati hiyo ambapo pindi boma litakapokamilika atachangia mabati yote yatakayohitajika kwa ajili ya kuezeka.

Dkt Tizeba alisema kuwa lengo la kuchangia mahitaji hayo ni kuakisi ahadi ya ujenzi wa zahanati katika kila kijiji ili kuboresha huduma za upatikanaji wa tiba kwa wananchi katika vijiji.

Mchango huo pia umejibu changamoto iliyoainishwa kwenye taarifa fupi ya kijiji na Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Bulyaheke Ndg Ezekiel Galula aliyeomba mchango wa mbunge huyo kufabikisha ujenzi wa zahanati.

Dkt Charles Tizeba ambaye ni Waziri wa kilimo amewataka wananchi hao kununua haraka dawa za kuua wadudu vamizi kwenye Mazao kwani kutofanya hivyo kutasababisha wadudu hao kuvamia mashamba yote.

Katika hatua nyingine Dkt Tizeba amepiga marufuku walimu kuwatumia wanafunzi kulima kwenye mashamba yao pamoja na kufanya shughuli binafsi za walimu huku akisisitiza kuwa kwa mashamba ambayo ya walimu ambayo tayari yamelimwa na 

MWISHO.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com