METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, May 9, 2018

RC MAKONDA ATOA ANGALIZO KWA WAKANDARASI "WAPIGAJI"

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Paul Makonda* amewaonya wakandarasi wenye tabia ya kutengeneza *Barabara za chini ya kiwango* na kuharibika ndani ya *muda mfupi* jambo linalosababisha *hasara kwa serikali* na usumbufu kwa watumiaji wa *vyombo vya usafiri.*

*RC Makonda* ametoa onyo hilo wakati wa hafla ya *utiaji wa saini kwa Mikataba Nane ya mradi wa matengenezo ya Barabara, Mifereji ya Maji na Culvets* inayotekelezwa na Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini *TARURA* yenye tahamani ya zaidi ya *Billion 5.8* ambapo amewataka *TARURA* kuhakikisha *wanasimamia ipasavyo* ujenzi wa barabara hizo.

Aidha *RC Makonda* amezitaja Barabara zitakazojengwa kupitika *mradi* huo kuwa ni pamoja na *Tegeta Nyuki, Msasani, Magomeni Makuti,Migombani, Kimara baruti, Kibanda cha Mkaa, Sheikh Bofu, Kwa Komba, Msigani, Sea clif na Mwananyamala Kisiwani.*

Hata hivyo *RC Makonda* ametoa *wiki mbili* kwa *TARURA* kuhakikisha wakandarasi waliojenga *barabara chini ya kiwango* zinajengwa *upya* kwa *gharama ya mkandarasi* ikiwemo *barabara ya Mabatini* ambapo barabara hizo zitakuwa na *mifereji ya maji, sehemu za watembea kwa miguu na Taa za Barabarani.*

Pamoja na hayo *RC Makonda* amesema katika *uongozi wake hawezi kufumbia macho matumizi mabovu ya fedha za walipa kodi* hivyo atahakikisha anasimama *kidete* kuhakikisha *Dar es salaam inakuwa na barabara zenye ubora.*

Sanajari na hayo *RC Makonda* ametaka uwepo wa ushirikiano wa kikazi baina ya *TARURA, TANROAD, TANESCO, DAWASCO na TTCL* ilikupunguza *ucheleweshaji* wa miradi na ujenzi usiofuata taratibu unaopelekea *uharibifu wa miundombinu.

LENGO LA RC MAKONDA NI KUHAKIKISHA PESA YA WALIPA KODI INATUMIKA KUONDOA KERO WANANCHI

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com