Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi,
Maliasili na Utalii imeipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kazi nzuri iliyofanya ya ujenzi wa jengo la makumbusho ya kisasa katika Bonde la Olduvai ya Gorge ambako ni chimbuko la
historia ya Binadamu.
Kamati hiyo imesema imeridhishwa na
ujenzi wa jengo hilo ambalo litawavutia watalii na wanasayansi wabobezi wa masuala ya Malikale kutembelea Makumbusho
hiyo.
Kamati hiyo ilibainisha kuwa Makumbusho hiyo mbali ya kutumika kuingiza pesa kupitia watalii pia inatumika kama kielelezo na utambulisho muhimu wa
taifa katika kutangaza utamaduni wa
Mtanzania ndani na nje ya nchi.
Hayo yalisemwa jana na Kamati hiyo wakati ilipofanya ziara ya kutembelea Ngorongoro Crater na Makumbusho ya Olduvai Gorge katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo. Kemilembe Luota
ameipongeza Serikali pamoja na wataalamu kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa
kuhakikisha kuwa eneo la Olduvai Gorge linakuwa
kivutio bora kwa ajili ya historia ya nchi na kivutio kikubwa cha Utalii
duniani.
‘’ Sisi kama
Kamati tunaipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kuyafanyia kazi
mapendekezo yote tuliyoyatoa kwa mara ya kwanza tulipokuja kwa vile tumeona
kazi nzuri imefanyika.’’
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo
ametoa wito kwa wananchi kutembelea makumbusho hiyo kwa vile idadi ya watalii wa ndani aliyokutana
nayo sio ya kuridhisha.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,
Japhet Hasunga amesema makumbusho hiyo inatoa ushahidi dhahiri kuwa hata wazungu, mababu zao walitoka Afrika.
Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye pia ni
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema
Makumbusho hiyo hadi hapo ilipofikia imeboreshwa kwa kiwango cha hali ya juu
hata hivyo ameitaka Wizara ihakikishe inaitangaza ipasavyo ili watalii wengi
zaidi wazidi kutembelea.
Awali, Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka hiyo,
FredyManongi amesema tangu kuzinduliwa
kwa makumbusho hiyo kwa wiki moja
imekuwa ikipokea zaidi ya watalii
wapatao 40000 hali inayopekelea kuwa ni
miongoni mwa Makumbusho inayofanya vizuri zaidi barani Afrika
0 comments:
Post a Comment