
Mkuu wa Mkoa Wa Pwani ,mhandisi Evarist
Ndikilo ,wa pili kushoto ,katibu tawala wilaya ya Kibaha Sozi Ngate wa
kwanza kulia ,pamoja na mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Kibaha
,Leonard Mloe wa pili kutoka kulia ,wakiwa wameshika tuzo ya kuwa wa
kwanza katika ufungaji wa mahesabu ya serikali kati ya halmashauri zote
nchini mwaka 2014/2015 iliyopatiwa halmashauri hiyo
Picha na Mwamvua Mwinyi
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
HALMASHAURI ya Mji wa Kibaha,mkoani
Pwani,imewachukulia hatua ya kinidhamu kwa kuwafukuza kazi watumishi 28
kwa makosa ya utoro kazini,kughushi vyeti na upotevu wa mali za
halmashauri.
Aidha halmashauri hiyo ,inakabiliwa na upungufu wa watumishi 164,ambapo uhaba mkubwa upo katika idara ya utawala ,maji na afya.
Licha ya upungufu huo,halmashauri hiyo
imekua ya kwanza katika ufungaji wa mahesabu ya serikali kwa mwaka
2014-2015 kati ya halmashauri 186 nchini.
Hayo aliyasema katibu tawala wa wilaya
ya Kibaha,Sozi Ngate kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo,wakati akitoa
taarifa ya maendeleo ya halmashauri hiyo katika ziara ya siku moja ya
mkuu wa mkoa wa Pwani,:’Alipotembelea baadhi ya miradi ikiwemo kituo cha
mabasi cha kisasa kitakachogharimu bilioni 3.4 na ujenzi wa jengo la
halmashauri hiyo.
Sozi alisema ,kati ya watumishi
waliofukuzwa kazi ni pamoja na walimu 20,watendaji watatu,tabibu
wawili,katibu muhtasi ,afisa ardhi na daktari mmoja.
Hata hivyo alieleza,ili kukabiliana na
upungufu wa watumishi halmashauri inategemea kuajiri watumishi 73 ambao
mishahara yao imetengwa na ofisi ya rais –utumishi na wizara ya fedha na
mipango kwa mwaka 2017/2018.
Akielezea zoezi la uhakiki wa vyeti vya
elimu,,Sozi alieleza ulifanyika kwa watumishi wote 1,529 ambapo
watumishi 73 wameondolewa kwa kukutwa na vyeti feki.
“Kwa upande wa uhakiki wa watumishi hewa
ulianzia machi 2016 hadi april,jumla ya watumishi 20 waligundulika ni
watumishi hewa na jumla ya fedha mil 19.161.557 ziliokolewa”alifafanua
Sozi.
KATIKA HATUA NYINGINE,akizungumzia
kuhusu ukusanyaji wa mapato ya halmashauri hiyo ,alisema wanaendelea
kusimamia ukusanyaji huo .
Sozi alisema mwaka 2016-2017 halmashauri
ilikadiria kukusanya zaidi ya sh.bil.3.954.4 katika vyanzo vya ndani na
makusanyo halisi hadi kufikia juni 30 mwaka huu ilifanikiwa kukusanya
sh.bil.3.671.950.5 sawa na asilimia 93.
Mwaka 2017-2018 halmashauri ya mji huo
imekisia kukusanya sh.bil.3.705.549 ambapo mapato halisi hadi septemba
30 ,2017 imekusanya sh.bil.1.431.090.552 sawa na asilimia 38.6 ya
makisio.
“Tusipojisifu wenyewe hakuna wa
kutusifia,tujipongeze halmashauri yetu imekuwa ya kwanza katika ufungaji
wa mahesabu ya serikali kwa mwaka 2014-2015 kati ya halmashauri zote
nchini ,
VIWANDA….Halmashauri ya mji Kibaha
inaendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ambapo katika robo ya
kwanza ya 2017/2018 imeweza kutumia mil.100 kufungua barabara eneo la
viwanda Zegereni na inaendelea kupokea maombi ya wawekezaji.
Sozi alielezea,mji huo una jumla ya
viwanda 119 vinavyofanya kazi kati ya hivyo vikubwa ni vitano,vya kati
16 na vidogo 98 huku viwanda vinne vinaendelea kujengwa .HATA HIVYO
,kuhusu soko jipya la Mnarani (Loliondo)alisema zimeshawekwa taa na
wameshatenga eneo la kujengwa kituo cha polisi .
MKUU WA MKOA WA PWANI,mhandisi Evarist
Ndikilo ,aliipongeza halmashauri hiyo kwa jitihada mbalimbali
wanazozifanya kimaendeleo.Alisema anaendelea kufuatilia maombi ya
halmashauri hiyo ya mji kuwa manispaa ambayo yalishayapelekwa TAMISEMI .
Mhandisi Ndikilo alisema ,mji huo unakua
siku hadi siku,huduma za kijamii zinaongezeka,idadi ya watu imeongezeka
hivyo vigezo vya mji kuwa manispaa vimeshafikiwa.“Mkoa wa Pwani
unaongoza katika kukuza uchumi wa viwanda ,nawaombeni tuongeze jitihada
kuboresha miundombinu ya maji,barabara na umeme kuvutia wawekezaji zaidi
ya sasa”alifafanua mhandisi Ndikilo.
Mhandisi Ndikilo,aliitaka halmashauri
hiyo kuweka ulinzi kwenye soko la Mnarani ili kulinda mali zao sokoni
hapo.Alisema kuna kila sababu ya kuweka mikakati ya muda mrefu na mfupi
ikiwemo kufanya doria za mara kwa mara usiku kwa ajili ya ulinzi,
kuwasaidia watu na mali zao.
Katika ziara yake mhandisi
Ndikilo,alitembelea ujenzi wa jengo la ofisi za halmashauri hiyo na
kituo cha mabus kipya kinachojengwa eneo la CBD kitakachogharimu bilioni
3.4 hadi kukamilika.
NAE meneja wa kampuni ya Group Six
International Ltd ,inayojenga kituo cha hicho ambayo ilijenga stendi ya
kisasa ya Msamvu mkoani Morogoro,mhandisi Chen Xlong ,alisema ujenzi
umefikia asilimia 45.
Alisema licha ya kuwa nyuma kidogo ya
wakati katika kukamilisha ujenzi huo lakini wanatarajia kukamilisha
ujenzi huo desemba mwaka huu.
Stendi hiyo itakuwa na uwezo wa
kuhudumia mabasi 60 kwa wakati mmoja na inajengwa kwa ufadhili wa bank
ya dunia kupitia fedha za ruzuku kwenye mradi wa uendelezaji wa miji
(ULGSP) unaoendeshwa kwenye miji 18 hapa nchini ikiwemo Mji wa Kibaha
0 comments:
Post a Comment