METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, October 6, 2017

WANANCHI WAFUNGUKA; WADAI WAMESUBIRI MUDA MREFU KUANZA KWA USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA – SHINYANGA

pic1
Watumishi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakiingiza taarifa za wananchi kwenye mfumo wakati wa zoezi la usajili linaloendelea katika ofisi ya kata ya Lubaga, Halmashauri ya Manispaa ya  Shinyanga.
pic2 pic3
Hawa ni baadhi tu ya wananchi ambao kamera yetu imewanasa wakisubiri huduma ya Usajili  katika zoezi linaloendelea la Usajili na Utambuzi wa Watu kwa lengo la kuwapatia Vitambulisho vya Taifa.
pic4
Kina mama na wazee waliojitokez kusajili katika Kata ya Lubaga wakisubiri kuitwa majina kuingia chumba cha Usajili kupata huduma.
……….
Wananchi mkoani Shinyanga wamesema wamefarijika kuona kuanza kwa zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa kwani ni zoezi ambalo wamekuwa wakilisikia kwa muda mrefu na hatimaye nao wamefikiwa na kupata fursa ya kujisajili.

Akizungumza wakati zoezi hilo likiendelea mmoja wa kutoka kata ya Lubaga Shinyanga Mjini amesema “kwa muda mrefu tulikuwa tukisubiri kuanza kwa zoezi hili kwani wananchi tunapata shida hususani wakati tukiwa tunataka kupata huduma mbalimbali ambazo zinalazimu mtu kuwa na Kitambulisho cha Taifa, hivyo hii ni fursa kwa wakazi wote wa Shinyanga kuweza kujitokeza Kusajiliwa”.

Baadhi ya huduma ambazo sasa zimeanza kutolewa wa kutumia Vitambulisho vya Taifa ni huduma ya kusajili namba za simu, Huduma za Benki, kutambulika kwenye huduma kwa Kaya masikini kirahisi na huduma nyinginezo.

Mkoa wa Shinyanga ni miongoni mwa mikoa katika Kanda ya Ziwa ambapo zoezi hilo linaendelea kwa sasa likihusisha uchukuaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya Kilelektroniki. Mikoa mingine ni Mara, Mwanza, Simuyu, Geita, Singida, Manyara, Kilimanjaro, Arusha, Mbeya na Songwe.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com