METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, September 16, 2017

KAMANDA MAMBOSASA: MAPAMBANO NA WAHALIFU YANAENDELEA

Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limeendelea na msako wa wahalifu sehemu mbalimbal za Jiji hilo na lufanikiwa kupatikana kwa silaha moja aina ya bastola na kuuwawa kwa majambazi watatu.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi kanda maalum Dar es Salaam SACP Lazaro Mambosasa amesema Jeshi la Polisi kanda maalum mnamo tarehe 13 mezi wa 9 mwaka huu majira ya saa tatu usiku huko Mbiku Chamazi lilifanikiwa kukamata silaha moja, bastola aina ya BERRETA yenye namba A065775Z ikiwa na risasi tano ndani ya magazine katika majibizano ya risasi kati ya Askari Polisi na majambazi wapatao watano.

“Silaha hiyo ilipatikana baada ya askari kupata taarifa ya kuwepo kwa njama za majambazi hao watano (5) kufanya uporaji katika maduka ya M-Pesa na Tigopesa eneo hilo, na hatimaye kuweka mtego eneo hilo ambapo askari walifanikiwa kuwaona majambazi hao wakishuka kwenye gari yao kwaajili ya kufanya tukio hilo” Alisema Kamanda Mambosasa.

Vile vile Kamanda Mambosasa ameongeza kwa kusema kuwa kuwa majambazi hao walipogundua wanafatiliwa na askari walianza kufyatua risasi kuwashambulia askari na ndipo askari walijibu mashambulizi na kufanikiwa kuwajeruhi majambazi watatu kati ya watano huku wengine wawili wakikimbia.

Aidha Kamanda Mambosasa ameeleza kuwa silaha hiyo aina ya bastola baada ya kupekuliwa, risasi tano zilikuwa ndani ya magazine, moja ilikuwa chemb tayari kwa kutoka huku maganda sita ya silaha hiyo yalipatikana eneo la tukio, huku majambazi waliojeruhiwa walifariki dunia baada ya kufikishwa hospitali ya Taifa Muhimbili ili kupatiwa matibabu, huku msaka mkali ukiendelea kuwatafuta majambazi wawili walio kimbia.

Kamanda Mambosasa pia ametoa katazo la mikusanyiko isiyo na kibali kutoka Polisi na ametoa onyo kali kwa watakaokiuka kwani hatua kalii za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com