METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, September 20, 2017

JAFO AWAPONGEZA VIONGOZI WA DINI DODOMA

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo amewapongeza viongozi wa dini kwakuwa mstari wa mbele katika kuliombea Taifa na kuwaomba kuendelea na moyo huo na kukemea vitendo viovu.

Jafo ameyasema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika semina ya siku tatu ya viongozi wa madhehebu mbalimbali ya kikiristo mkoani Dodoma.

Naibu Waziri Jafo amewaomba viongozi hao wa dini kuendelea kusimamia maadili kwa kuendelea kukemea matendo maovu yakiwemo matumizi ya madawa ya kulevya, rushwa na mauaji ya vikongwe.

Aidha Jafo amewaomba viongozi hao wa dini kupinga mambo yote yasiyo mpendeza mungu.

Akizuzungumzia kuhusu amani na utulivu hapa nchini, Jafo amesema kwasasa nchi inapoelekea katika uchumi wa viwanda ni vyema viongozi hao wakaendelea kuliombea Taifa kwa kuwa bila amani malengo hayawezi kufikiwa.

“Nawaomba pia muendelee kumuombea Rais wetu Dk. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayo ifanya kwa manufaa ya wananchi wote,”amesema Jafo

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiongea na viongozi wa dini mjini Dodoma

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa dini
Wanasemina wakifuatilia maelekezo katika semina ya siku tatu ya viongozi wa madhehebu ya dini mkoani Dodoma
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com