Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Dkt. Medard Kalemani amesema kuanzia Agosti 30 mwaka huu, Serikali
itatangaza zabuni ya kuanza ujenzi wa Mradi Mkubwa wa Umeme wa megawati
2100 katika maporomoko ya maji ya Mto Rufiji mkoani Pwani ( Stiegler’s
Gorge).
Akizungumza jijini Dar es Salaam
Dkt. Kalemani amesema, taratibu za awali zimeshaanza ambapo
wataalaumu wa ndani na nje wameshakutana na kuchagua sehemu za kujenga
mradi huo katika Mto Rufiji, ambapo tayari Shirika la Umeme Nchini (
Tanesco ) limeanza upembuzi yakinifu wa kujenga miundombinu ya umeme na
Wakala wa barabara nchini (Tanroad) kujenga miundombinu ya barabara.
Ujenzi wa mradi wa umeme wa
megawati 2100 kutoka maporoko ya maji ya Mto Rufiji Mkoani Pwani (
Stiegler’s Gorge)unatarajiwa kuanza ndani ya kipindi cha miezi miwili
ijayo baada ya taratibu za zabuni kukamilika, Naibu Waziri wa Nishati na
Madini Dkt. Medard Kalemani amewambia watanzania kuwa, tayari Serikali
imetenga fedha za kutekeleza mradi huo, na hatua za awali za utekelezaji
zimekwisha fanyika, ambapo tarehe 30 ya mwezi huu wa Agosti Serikali
itatangaza zabuni kwa wakandarasi wa ndani na nje ya nchi ili waweze
kuomba kufanya kazi .
Dkt. Kalemani amesema mkandarasi
atakayepewa kazi ya kujenga mradi huo ni yule tu atayeridhia kujenga kwa
gharama nafuu na kwa muda mfupi zaidi ya uliowekwa.
Pia Dkt. Kalemani anatoa ufafanuzi namna ambavyo Serikali imejiandaa katika kutekeleza mradi huo.
Kwa mujibu wa Dkt Kalemani, mradi
huo utakapokalimilika utakasaidia kuimarisha upatikanaji wa huduma ya
umeme nchini na kwamba Serikali haitarajii kuongeza bei ya umeme.
0 comments:
Post a Comment