Majadiliano
kati ya kamati maalumu iliyoundwa na Rais John Magufuli na wawakilishi
kutoka kampuni ya Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini
yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo nchini yameanza leo, Julai 31
jijini Dar es Salaam.
Taarifa
ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imesema
kamati ya Tanzania inaongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa
Palamagamba Kabudi.
Imesema kamati kutoka Barrick inaongozwa na Ofisa Mwendeshaji Mkuu, Richard Williams.
Profesa
Kabudi amekaririwa katika taarifa hiyo akisema wamejipanga vizuri
kujadiliana na Barrick juu ya madai ya Tanzania katika biashara ya
madini ya kampuni hiyo nchini na itahakikisha inasimamia masilahi ya
nchi ipasavyo.
Williams imeelezwa ameshukuru uwepo wa majadiliano
hayo, akisema Barrick imepokea madai ya Tanzania kwa mtazamo chanya na
ipo tayari kujadiliana na kufikia makubaliano yenye masilahi kwa pande
zote mbili.
Rais aliunda kamati hiyo baada ya kupokea ripoti za
kamati zingine mbili, moja ilichunguza mchanga wa madini (makinikia) na
nyingine ya kitaalamu iliyochunguza masuala ya kisheria na kiuchumi
kuhusu mchanga huo unaosafirishwa nje ya nchi.
Monday, July 31, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa upinzani, Kizza Besigye akisindikizwa na maofisa wa gereza la Luzira alikokuwa akishikiliwa Kiongozi w...
-
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa, ambaye pia ni Mnec wa Mkoa wa wa Iiringa Salim Asas akimkabidhi Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Kilo...
-
Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akionyesha mfuko mtupu uliogushiwa na kiwanda cha Global Packaging limited wakati akizungumza n...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
-
Na Saida Issa, Dodoma CHAMA Cha wafugaji Tanzania (CCWT)kimewataka wafugaji kuhudhuria mkutano wa dharura kufuatia barua iliyotoka ofisi ya ...
Powered by Blogger.





0 comments:
Post a Comment