METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, May 16, 2017

TAARIFA KWA WANA UVCCM - WILAYA YA UBUNGO

Jumanne 16 May 2017

Leo tulikuwa na kikao cha watendaji wa UVCCM wa  Kata zote kumi na nne (14) zinazounda Wilaya ya UBUNGO.

Tumekutana na kujadili mambo mbalimbali kwa ujenzi wa jumuiya zetu na kusimamia kanuni na miongozo inayotuongoza bila kuangalia dini, cheo, kabila wala sura ya mtu yeyote.

Kwa sasa tupo katika mchakato wa uchaguzi kwa hiyo  tunapaswa kuwa  makini, tutende haki, tushiriki kwa ukamilifu.

Pia wana UVCCM  sikilizeni maelekezo ya viongozi wenu wa matawi yanayotoka Kata.

ANGALIZO

Kupanga uongozi (safu) ni kosa ambalo hatua zake hazitaangalia nani kapanga bali KANUNI YA MAADILI YA VIONGOZI ya 2012 itachukua nafasi yake.

Vijana ndio jeuri ya chama, sio kwa kukiuka kanuni na maadili tuliyojiwekea, bali kwa kukifanya chama kipate nguvu na uhai zaidi, sababu sisi tuna nguvu ya kufanya mambo mengi mazuri na kwa haraka.

Kauli mbiu, VIJANA TUKUTANE SITE

LEAH D. MBEKE
K/UVCM - UBUNGO
DAR ES SALAAM

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com