BMGHabari
Lile tamasha la burudani la Nyanza Festival 2017, lililopaswa kufanyika hii leo April 16,2017 katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza limeahirishwa kwa kile kinachodaiwa kwamba ni aliyepewa tenda ya muziki kuingia mitini.
"Taarifa Muhimu, Tamasha la Nyanza Festival limeahirishwa kutokana na sababu zisizozuilika na litafanyika baada ya wiki mbili yaani 29/4/2017". Amebainisha mratibu wa tamasha hilo, Fabian Fanuel.
Awali Afisa Habari wa Nyanza Festival 2017, George Binagi, alibainisha kwamba zaidi ya wasanii 30 kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa tayari wamethibitisha kupanda jukwaa la Nyanza Festival 2017 hivyo niwasihi wapenzi wa burudani wakae tayari kwa burudani hiyo ambapo kiingilio itakuwa elfu tano tu.
Nyanza Festival ni tamasha lililoasisiwa na Wanatasnia mbalimbali kutoka Kanda ya Ziwa wakiwemo wanamuziki, watangazaji, waandishi wa habari, Madjz na wadau wengine wengi kupitia umoja wao wa Mwanza.Com chini ya kampuni ya Famara Entertainment, lengo likiwa ni kuukuza na kuuendeleza zaidi muziki wa Kanda ya Ziwa.
Monday, April 17, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
Na Debora Charles (Mtakwimu) Sensa ya watu na makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua, kutathimini na kuchapisha na kusamba...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
-
Na Lucas Raphael,Tabora Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora kwa mara ya kwanza imebatilisha hati ya Mashitaka na kuwahukumu kifungo c...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment