METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, April 13, 2017

MAKAMU WA RAIS ATAKA KIKOSI KAZI CHA KUNUSURU MTO RUAHA MKUU KUFANYA KAZI KWA UFANISI, AWATAKA WANAHABARI KUSHIRIKI KUELIMISHA JAMII

IMG_20170411_133956
Mkurugenzi  mkuu  wa TANAPA  Dkt Allan  Kijazi  akichangia  mada  kuhusu  uhifadhi wa  mto  Ruaha mkuu
Makamu  wa Rais  Samia Suluhu  Hassan  kulia  akiteta  jambo na  mkuu  wa  mkoa wa Iringa Amina Masenza na  waziri wa ardhi ,nyumba na maendeleo ya makazi leo
Mkuu  wa wilaya ya  Iringa  Richard Kasesela  akichangia  mada  juu ya  uhifadhi wa mto  Ruaha mkuu
washiriki  wa mkutano  huo  wakitoa maoni yao
Mbunge  wa  Mary Mwanjelwa  akichangia katika mkutano  huo
Waziri  wea Mazingira na muungano January Makamba akipokea  maelekezo toka kwa makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan leo
Aliyekuwa  mkuu wa mkoa wa Mbeya Abas Kandoro  akichangia jinsi ya  kulinda mto Ruaha mkuu
Waziri  wa Maliasili na utalii Dkt Jumanne Maghembe akifafanua jinsi ya  kuungana kulinda  maji kwa  faida ya wananchi na  wananya
Mbunge wa Makete Dkt  Norman Sigalla

Na MatukiodaimaBlog

MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan ametaka kikosi kazi kilichoundwa na ofisi yake kufanya kazi ya kunusuru mto Ruaha mkuu.

Akizungumza leo wakati wa mkutano wa kwanza wa kuhifadhi Ikolojia ya mto Ruaha alisema kuwa uwepo wa kikosi kazi hicho ni kuacha maneno na kuonyesha utendaji.

Alisema lengo la kuunda kikosi kazi hicho bila kwa sasa kushirikisha sekta binafsi ni kutaka kufagia nyumba yetu na kuona kasoro zilizojitokeza na baada ya hapo watashirikisha sekta binafsi.

Kwani alisema ushirikishwaji wa sekta zote ni muhimu kwa ajili yakunusuru mto Ruaha mkuu.
Huku akitaka wanahabari kushirikiana na kikosi kazi kuandaa vipindi vya elimu ya uhifadhi wa mto Ruaha mkuu na kuvirusha kwa wananchi.

Hata hivyo alisema kuwa kuwepo kwa kikosi kazi hicho hausimamishi sheria zilizopo katika uhifadhi wa mazingira na kutaka wizara zote kuungana kusimamia sheria za usimamizi bora wa maji.

Alisema kutokana na mgongano uliopo wa kila wizara kutetea eneo lake serikali imepoteza pesa nyingi sana katika uhifadhi na hivyo kutaka kuanzia sasa wizara zote kuungana kunusuru mto Ruaha mkuu.

Aidha alisema anaunga mkono wazo la mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliam la kutaka kuangalia pia mito midogo.

Hata hivyo alitaka watumishi wote wanaoshindwa kutimiza wajibu wao kama mabwana shamba, misitu na wengine kufanya kazi kulingana na pesa wanazolipwa na kuwa serikali itaweka usimamizi sahihi kuona kila mmoja analipwa kulingana na kazi.

“Ni imani yangu kuwa kikosi kazi hiki cha kunusuru mto Ruaha kitafanya kazi yake vizuri “
Alisema kuwa Papa  Francis alipata kusema kuwa Mungu ukimkosea atakusamehe ukitubu ila mazingira ukiyakosea hayatakusamehe.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com