METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, March 13, 2017

TBL Group Na Mkakati Wa kuingiza Sokoni Bia Za Gharama Nafuu

MKUH
Mkurugenzi wa TBL Group na Rais mwa Masoko kanda ya Afrika Mashariki akitoa ufafanuzi katika warsha ya udhibiti wa bia haramu iliyoandaliwa na kampuni hiyo
MKUH 1
Moja ya kipeperushi kinachoelezea ubora kwa kinywaji cha Chibuku
MKUH 3
Watumiaji wa bia ya Chibuku wakifurahia baada ya  kazi
MKUH 4
TBL Group imekuwa mstari wa mbele kuwezesha wakulima kwa ajili ya kupata malighafi  ikiwemo zabibu na Shahiri 

Chibuku na Balimi zazidi kukubalika kama bia za kitanzania na zilivyotengenezwa na malighafi yaTanzania

Wakati tafiti zinabainisha kuwa bia zinazotengenezwa nchini Tanzania zinauzwa kwa bei kubwa ambayo watumiaji wengi hawana uwezo wa kumudu kuzinunua,kampuni ya TBL Group inaendeleza mkakati wake wa kuhakikikisha inaimarisha masoko ya bia ya asili ya Chibuku ikiwemo kutengeneza bia kwa kutumia malighafi zenye unafuu wa bei ili kuwezesha watumiaji wengi kumudu kuzinunua.

Mkakati huo ulibainishwa katika warsha ya siku moja kuhusu udhibiti wa pombe haramu iliyoandaliwa na TBL Group jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya vinywaji na watendaji kutoka taasisi za serikali liyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Wadau kutoka sekta ya vinywaji walieleza bayana kuhusu changamoto kubwa wanayokabiliana nayo katika soko ya kuuza bia kwa bei kubwa zinazosababishwa na gharama kubwa za uzalishaji ikiwemo kodi kubwa wanazotozwa kuanzia kwenye malighafi mpaka kwenye bidhaa.

Mkurugenzi Mkuu wa TBL Group,Roberto Jarrin, ambaye pia ni Mkuu wa Masoko katika ukanda wa Afrika Mashariki ,alisema kuwa kampuni yake imejizatiti kutengeneza na kuimarisha soko la bia za gharama nafuu kama ambavyo inaendelea kuwekeza katika bia ya asili ya Chibuku.

Alisema kuwa bia ya Chibuku umaarufu wake umekuwa ukiongezeka siku hadi siku na kutumiwa na wananchi wengi kutokana na kuwa na unafuu wa bei unaoendana sambamba na vipato vya watanzania wengi na inatengenezwa katika mazingira bora na kuwekwa kwenye vifungashio vya kisasa kulinganisha na bia nyingine za asili ambazo zinapatikana katika mazingira yasio salama.


Utafiti uliofanywa na kampuni ya kimataifa ya utafiti wa matumizi ya bidhaa kwa walaji ya CanBack umebainisha kuwa matumizi ya pombe za asili unatawala soko la  vinywaji vyenye kilevi Tanzania kwa asilimia 50%.  “kutokana na ripoti ya  utafiti huo wa kitaalamu,TBL Group  imeboresha zaidi vinywaji vya asili aina ya Chibuku na Nzagamba  vinavyotengenezwa na viwanda vyake vya DarBrew ambapo vinapatikana kwenye chupa za ukubwa wa aina mbalimbali kuwawezesha wateja kuvipata katika mazingira ya usafi wakati huohuo kulingana na uwezo wa vipato vyao”Alisema.

Aliongeza kusema kuwa kupitia vinywaji hivi kampuni imeanzisha mpango unaojulikana kama ‘Chibuku Mamas’ wa kuwawezesha wanawake  kuviuza na kujipatia mapato ambapo mpaka kufikia sasa  unaendelea kuwanufaisha Wanawake wengi kiuchumi wakati huohuo kulinda afya za watumiaji wa pombe za asili waliokuwa wanatumia pombe zisizotengenezwa katika  mazingira salama “.Alisema Jarrin.

Wakati kampuni inayo mkakati wa kuimarisha masoko ya vinywaji vyake utafiti uliofanyika katika  mabaa mbalimbali jijini unabainisha kuwa mbali na bia ya asili ya Chibuku bia zingine zinazouzwa kwa bei nafuu ikiwemo bia ya Balimi hivi zinazidi kushika kasi kwa kuwa na watumiaji wengi ambapo pia wanazifurahia kutokana na uasili wake wa  kutengenezwa na malighafi ya mazao ya mtama na mahindi kutoka hapa nchini.

Bia nyingine za TBL ambazo zinatamba kwenye soko nchini baadhi yake ni Safari, Kilimanjaro, Ndovu, Castle Lager na Castle Lite .Kampuni pia imekuwa kinara wa kutengeneza vinywaji vikali na mvinyo ambavyo navyo vinatamba katika soko kwa asilimia 73% baadhi yake vikiwa ni   – Konyagi za Chupa, Valeur za chupa na Dodoma Wine.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com