METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, March 16, 2017

Mji wa Magumeri Nigeria washambuliwa na Boko haram


                            Washambuliaji wa Boko Haram watekeleza shambulio
Ripoti kutoka kaskazini mwa Nigeria, zasema kuwa watu waliokuwa na silaha na wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la kiislamu la Boko Haram, wametekeleza shambulio katika mji wa Magumeri.

Duru zasema kuwa waliwashambulia raia kiholela huku wakiteketeza majumba yao.
Kuna ripoti inayosema kuwa, moshi mkubwa unaonekana ukifuka kutoka eneo ambalo kituo cha polisi kiko mjini humo.

Jeshi la Nigeria halijatoa taarifa zozote kuhusiana na shambulio hiloambapo Awali wanawake wanne walipuaji wa kujitolea kufa walijilipua katika mji ulioko karibu wa Maiduguri, na kusababisha vifo vya watu wawili.

Jimbo la Borno, limekumbwa na maafa mabaya na uhasama kati ya majeshi ya serikali na Boko Haram kwa muda wa miaka minane sasa

Boko Haram ni kundi la Waislamu wenye itikadi kali kaskazini mwa Nigeria ambalo lina mwelekeo wa kijihadi na hutumia mbinu za kigaidi katika kuekeleza mashambulizi yake .

Boko Haram ilianzishwa na Yusuf Mohamed mwaka 2002 na inalenga kuanzisha dola la Kiislamu katika Nigeria ambako ni sheria ya pekee

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com