WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa
amewataka wadau wa usafirishaji kuweka mikakati thabiti ya kupunguza
ajali za barabarani nchini ili kuokoa maisha ya Watanzania.
Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano Maalumu
wa Kanda wa kujadili na kutathmini changamoto za usalama barabarani na
jinsi ya kuzikabili uliowashirikisha wadau mbalimbali wa usalama
barabarani kutoka ndani na nje ya nchi.
Alisema ajali za barabarani zimekuwa zikikatisha maisha ya Watanzania
wengi wakiwamo vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa, hivyo ni jukumu la
wadau kuondoa hali hiyo.
“Kama tukijifunza vizuri na kuyafanyia kazi mafunzo haya tunaweza
kubadili hali ya usalama barabarani kwani inaumiza kuona vifo vya watu
wengi vinavyotokana na ajali za barabarani hivyo ni wakati wa Jeshi la
Polisi, na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini
(Sumatra) kushirikiana kukomesha ajali hizi,” alisema.
Mwenyekiti wa Mfuko wa Barabara Tanzania (RFB), Joseph Haule alisema
Bodi hiyo inashirikiana na taasisi nyingine katika kuhakikisha
miundombinu ya barabara inakuwa salama na kupitika wakati wote.
Alisema kama jitihada madhubuti hazitachukuliwa kwa haraka
inakadiriwa kwamba vifo vinavyotokana na ajali vinaweza kuongezeka kwa
asilimia sita kwa mwaka kutokana na kuongezeka kwa vyombo vya moto huku
akisema wanaume ndiyo waathirika wakubwa wa hilo.
Mapema Mwenyekiti wa Shirikisho la Kimataifa la Barabara (IRF), Kiran
Kapila alisema zaidi ya Dola za Marekani trilioni 1.8 zinapotea kila
mwaka kutokana na ajali za barabarani na kuziomba serikali kuchukua
hatua kukabiliana na tatizo hilo.
Tuesday, March 14, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samuel Jeremia Opulukwa akinawa mikono kabla ya kuingia katika Zahanati ya Saza itakayotumika kutibu endapo ata...
-
MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Tanzania (DCI), Robert Boaz Mikomangwa amesema Jeshi la Polisi nchini Tanzania na vyombo vingi...
-
Naibu waziri Kilimo Mhe. Omari T. Mgumba (Mb) akiwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa arusha alipokutana na wataalamu wa kilimo ,ushirika na ...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment