METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, March 14, 2017

AJALI MBAYA YATOKEA SHINYANGA BASI LA ABIRIA NA GARI NDOGO YAGONGANA USO KWA USO


Wakati serikali kupitia jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani wakijitahidi kutoa elimu ya usalama na matumizi sahihi ya barabara bado kumekuwa na ongezeko kubwa la ajali za barabarani ambapo leo basi lenye namba za usajiri T636AWC mali ya kampuni ya  RUKSA CLASSIC likitoka jijini Mwanza kwenda Mkoani Kigoma limegongana uso kwa uso na gari dogo lenye namba za usajiri T 210 DJJ katika kijiji cha Nhelegani  mkabala na chuo cha Ushirika Moshi kambi ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga.
                    GARI LA RUKSA LIKIWA LIMEGONGANA NA GARI NDOGO
Ajali giyo imetokea majira ya nne asubuhi huku chanzo chake kikielezwa kuwa    ni uzembe wa dereva wa gari ndogo ambaye hakuwa na utulivu barabarani na kujikuta yupo upande usio sahihi na kusababisha ajali.
Hata hivyo hakuna mtu aliyepoteza maisha ingawa dereva wa gari dogo na abiria wake mmoja, wameumia na kukimbizwa katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga.
 
MASHUHUDA WAKIANGALIA AJALI HIYO
 
 HAPA GARI ILIYOSABABISHA AJALI IKIWA KATIKA HALI MBAYA
 
 
 
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com