DAKTARI David Mapunda kutoka Chama cha Madaktari wa Vinywa na Meno
Tanzania (TDA), amewashauri baadhi ya wananchi wenye kutumia majivu,
mkaa na sabuni kuoshea vinywa vyao na meno, waache mara moja kwani
vinaleta madhara ya kuharibu mishipa ya fahamu.
Daktari huyo alisema hayo mjini Shinyanga wakati wa kutoa ushauri na
tiba katika kituo jumuishi, kinacholea watoto wenye ulemavu mbalimbali
kilichopo Buhangija, ikiwa matibabu hayo yalikuwa yamelenga kwa watoto
wenye ualbino wenye kuishi kwenye kituo hicho.
Dk Mapunda alisema matumizi ya vitu hivyo, siyo sahihi kwa afya ya
kinywa na madhara yake ni kuharibu meno na mishipa ya fahamu, sababu
mikaa na majivu huwa sio laini, inaweza kuleta madonda ya mchubuko
katika kinywa, jambo ambalo pia ni hatari.
Alisema wapo baadhi ya wananchi hasa wa vijijini, hupenda kusukutua
au kuosha kinywa hususani meno kwa majivu, sabuni na mkaa, wakiamini
wapo salama.
“Baadhi ya wamekuwa wakitumia majivu, sabuni na mkaa kusafisha meno
kwa imani kuwa vitu hivi hutumika kuondoa uchafu, bila ya kufahamu ni
hatari kwa afya ya vinywa vyao elimu na ushauri tunaendelea kuvitoa kila
mahali,” alisema Dk Mapunda.
Aidha, alisema dawa za meno zilizothibitishwa kitaalamu, ndio sahihi
kwa matumizi ya kusafisha kinywa na kinga ya meno, sababu huwa zina
madini ya florine ambayo humfanya mtu kuwa salama.
Rais wa Madaktari wa Chama cha Kinywa na Meno Tanzania, Dk Lorna
Carneiro akizungumza wakati wakitoa huduma ya kutibu meno kwa watoto
albino mjini Shinyanga, alisema watajitahidi kutoa elimu ya afya ya
kinywa maeneo yote ya vijijini.
Pia Dk Carneiro alitoa mwito kwa Serikali ya Mkoa wa Shinyanga,
kuendeleza huduma hiyo ya kutibu afya ya kinywa na meno kwa watoto hao
hasa waliokuwa wamelengwa wenye ualbino ikiwa mkataba wao wa miaka
mitatu umefika kikomo.
Mlezi Mkuu wa Kituo hicho jumuishi, Suleiman Kipanya alikipongeza
chama hicho kwa kutoa huduma ya kinywa na meno ndani ya miaka mitatu
mfululizo kwa watoto hao na kuwafanya meno yao kuendelea kuwa imara.
Credit:Habari Leo
Wednesday, March 15, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda akizungumza na watumishi wa Mkoa wa Rukwa (hawapo pichani) Wakuu wa taasisi mba...
-
MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Tanzania (DCI), Robert Boaz Mikomangwa amesema Jeshi la Polisi nchini Tanzania na vyombo vingi...
-
Naibu waziri Kilimo Mhe. Omari T. Mgumba (Mb) akiwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa arusha alipokutana na wataalamu wa kilimo ,ushirika na ...
-
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akitoa taarifa ya miaka minne ya uzalishaji wa zao la Korosho nchini am...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment