WAGONJWA 11 wamefanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalumu ya
matibabu ya moyo, inayofanywa na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo
kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ushirikiano na
madaktari wenzao wa Taasisi ya Open Heart International ya Australia.
Taarifa iliyotolewa na JKCI, ilimkariri Mkurugenzi wa Upasuaji wa
Moyo ambaye pia ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo, Dk Bashir
Nyangasa wakati akielezea jinsi kambi hiyo ya upasuaji inavyoendelea
kutoa matibabu kwa wagonjwa.
Dk Nyangasa alisema, “Kwa kushirikiana na washirika wetu wa OHI
tulianza kambi maalum ya upasuaji kuanzia tarehe kumi mwezi huu wa tatu
hadi leo tarehe kumi na nne (jana), tumefanya upasuaji kwa wagonjwa kumi
na moja ambao wanaendelea vizuri. Kati ya hao watoto ni tisa na watu
wazima ni wawili.”
Alisema katika kambi hiyo ambayo inamalizika Machi 17, mwaka huu,
walipanga kufanya upasuaji kwa wagonjwa 25 kati ya hao watoto ni 15 na
watu wazima ni 10.
Kuhusu mahitaji ya damu kwa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo,
Dk Nyangasa alisema wagonjwa hao wanahitaji damu nyingi, hivyo aliwaomba
wananchi wajitokeze kuchangia damu, ambayo itatumika kwa wagonjwa.
“Tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kuchangia damu na uchangiaji
huu wa damu usifanyike mara moja bali uwe endelevu kwani Taasisi inatoa
huduma kwa wagonjwa wakati wote siyo wakati wa kambi maalum za matibabu
ya moyo pekee yake,” alisisitiza Dk Nyangasa.
Tangu kuanza kwa mwaka huu, JKCI kwa kushirikiana na baadhi ya
washirika wake wa nje ya nchi ambao ni Madaktari Afrika wa Marekani,
Hospitali za Apollo, Bangalore na BLK zote za India na Open Heart
International ya Australia, wamefanya matibabu ya moyo ya kufungua na
bila kufungua kifua kwa wagonjwa wa moyo wanaotibiwa katika taasisi
hiyo.
Credit: Habari Leo
Wednesday, March 15, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Anna Joram Gidarya, amewataka wananchi wa Wilaya ya Busega kutoa maoni kwa uhuru kuhusu ombi la k...
-
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Angeline Mabula akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi mkoani Iringa wakati wa z...
-
Waziri wa kilimo Mhe Japhet Ngailonga Hasunga (Mb) Naibu Waziri wa Wizara ya kilimo Mhe Innocent Lugha Bashungwa Na Mathias C...
-
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Laigwnani Metui Ole Shaudo mapendekezo ya Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro kuhusu namna bor...
Powered by Blogger.

0 comments:
Post a Comment