WAGONJWA 11 wamefanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalumu ya
matibabu ya moyo, inayofanywa na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo
kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ushirikiano na
madaktari wenzao wa Taasisi ya Open Heart International ya Australia.
Taarifa iliyotolewa na JKCI, ilimkariri Mkurugenzi wa Upasuaji wa
Moyo ambaye pia ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo, Dk Bashir
Nyangasa wakati akielezea jinsi kambi hiyo ya upasuaji inavyoendelea
kutoa matibabu kwa wagonjwa.
Dk Nyangasa alisema, “Kwa kushirikiana na washirika wetu wa OHI
tulianza kambi maalum ya upasuaji kuanzia tarehe kumi mwezi huu wa tatu
hadi leo tarehe kumi na nne (jana), tumefanya upasuaji kwa wagonjwa kumi
na moja ambao wanaendelea vizuri. Kati ya hao watoto ni tisa na watu
wazima ni wawili.”
Alisema katika kambi hiyo ambayo inamalizika Machi 17, mwaka huu,
walipanga kufanya upasuaji kwa wagonjwa 25 kati ya hao watoto ni 15 na
watu wazima ni 10.
Kuhusu mahitaji ya damu kwa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo,
Dk Nyangasa alisema wagonjwa hao wanahitaji damu nyingi, hivyo aliwaomba
wananchi wajitokeze kuchangia damu, ambayo itatumika kwa wagonjwa.
“Tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kuchangia damu na uchangiaji
huu wa damu usifanyike mara moja bali uwe endelevu kwani Taasisi inatoa
huduma kwa wagonjwa wakati wote siyo wakati wa kambi maalum za matibabu
ya moyo pekee yake,” alisisitiza Dk Nyangasa.
Tangu kuanza kwa mwaka huu, JKCI kwa kushirikiana na baadhi ya
washirika wake wa nje ya nchi ambao ni Madaktari Afrika wa Marekani,
Hospitali za Apollo, Bangalore na BLK zote za India na Open Heart
International ya Australia, wamefanya matibabu ya moyo ya kufungua na
bila kufungua kifua kwa wagonjwa wa moyo wanaotibiwa katika taasisi
hiyo.
Credit: Habari Leo
Wednesday, March 15, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
Na Debora Charles (Mtakwimu) Sensa ya watu na makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua, kutathimini na kuchapisha na kusamba...
-
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono Wananchi wa Hai mara baada ya kuwasili Bo...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment