Mfumuko nchini Nigeria huenda umeathiri kampuni ya Dangote Group inayomilikiwa na mtu tajiri zaidi barani Afrika Aliko Dangote.
Kampuni hiyo imeripotiwa kuwafuta kazi wafanyikazi 48 wakiwemo wataalam 36 wa kigeni na raia 12 wa Nigeria.
Ripoti zinasema kuwa hatua hiyo inatokana na gharama ya juu ya kufanya
biashara katika taifa hilo na kampuni hiyo imeshindwa kupata fedha za
kigeni kuwalipa wafanyikazi hao wa kigeni.
Lakini msemaji wa Dangote Group Tony Chiejina aliambia BBC kwamba ufutaji huo hauna uhusiano na mfumuko.
Kampuni hiyo inasema kuwa ilikuwa inaimarisha biashara zake na kwamba kazi zengine zimechukuliwa na kampuni tanzu.
Kampuni ya Dangote Group ni miongoni mwa kampuni zilizo na wafanyikazi wengi katika sekta hiyo.
Miezi miwili iliopita ,kitengo cha habari cha Bloomberg kiliripoti
kwamba bwana Dangote alipoteza dola bilioni 5.4 mwaka huu kutokana na
kuanguka kwa thamani ya sarafu ya Nigeria ,Naira.
Monday, October 24, 2016
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Na Mathias Canal, Dodoma Utangulizi : Mradi wa kufua umeme kwa kutumika nguvu ya maji katika mto Rufuji uliopewa jina la ‘Julius Nyerere...
-
Kiongozi wa upinzani, Kizza Besigye akisindikizwa na maofisa wa gereza la Luzira alikokuwa akishikiliwa Kiongozi w...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
-
Na Hamis Hussein - Singida Serikali imetoa shilling bilioni 5.9 kwaajili ya kuendeleza ujenzi wa majengo mapya ya hospitali ya rufaa y...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
Powered by Blogger.

0 comments:
Post a Comment