Mfumuko nchini Nigeria huenda umeathiri kampuni ya Dangote Group inayomilikiwa na mtu tajiri zaidi barani Afrika Aliko Dangote.
Kampuni hiyo imeripotiwa kuwafuta kazi wafanyikazi 48 wakiwemo wataalam 36 wa kigeni na raia 12 wa Nigeria.
Ripoti zinasema kuwa hatua hiyo inatokana na gharama ya juu ya kufanya
biashara katika taifa hilo na kampuni hiyo imeshindwa kupata fedha za
kigeni kuwalipa wafanyikazi hao wa kigeni.
Lakini msemaji wa Dangote Group Tony Chiejina aliambia BBC kwamba ufutaji huo hauna uhusiano na mfumuko.
Kampuni hiyo inasema kuwa ilikuwa inaimarisha biashara zake na kwamba kazi zengine zimechukuliwa na kampuni tanzu.
Kampuni ya Dangote Group ni miongoni mwa kampuni zilizo na wafanyikazi wengi katika sekta hiyo.
Miezi miwili iliopita ,kitengo cha habari cha Bloomberg kiliripoti
kwamba bwana Dangote alipoteza dola bilioni 5.4 mwaka huu kutokana na
kuanguka kwa thamani ya sarafu ya Nigeria ,Naira.
Monday, October 24, 2016
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa amefunga mashindano ...
-
Waziri wa Kilimo Mhe Hasunga (Mb) Mwenye Tai, akiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa kampuni mbalimbali zinazojihusisha na uzalish...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
Ndugu zangu, Naomba nianze na tungo hii fupi... " Sina sauti nzuri ya kuimba, siwezi kucheza muziki watu wakanista...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment