Mfumuko nchini Nigeria huenda umeathiri kampuni ya Dangote Group inayomilikiwa na mtu tajiri zaidi barani Afrika Aliko Dangote.
Kampuni hiyo imeripotiwa kuwafuta kazi wafanyikazi 48 wakiwemo wataalam 36 wa kigeni na raia 12 wa Nigeria.
Ripoti zinasema kuwa hatua hiyo inatokana na gharama ya juu ya kufanya
biashara katika taifa hilo na kampuni hiyo imeshindwa kupata fedha za
kigeni kuwalipa wafanyikazi hao wa kigeni.
Lakini msemaji wa Dangote Group Tony Chiejina aliambia BBC kwamba ufutaji huo hauna uhusiano na mfumuko.
Kampuni hiyo inasema kuwa ilikuwa inaimarisha biashara zake na kwamba kazi zengine zimechukuliwa na kampuni tanzu.
Kampuni ya Dangote Group ni miongoni mwa kampuni zilizo na wafanyikazi wengi katika sekta hiyo.
Miezi miwili iliopita ,kitengo cha habari cha Bloomberg kiliripoti
kwamba bwana Dangote alipoteza dola bilioni 5.4 mwaka huu kutokana na
kuanguka kwa thamani ya sarafu ya Nigeria ,Naira.
Monday, October 24, 2016
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Mmoja wa Viongozi wa kikundi cha Hamasa cha Timu ya Tanzania Prison Stephen Rheda (aliyesimama) akitoa nasaha za mwisho kwa washabiki wenzie...
-
Na. Antonia Mbwambo, Arusha. Watumishi wa Umma nchini wamehakikishiwa kuboreshewa mazingira ya kazi kadri uchumi utakavyoruhusu ili kuleta ...
-
Na Debora Charles (Mtakwimu) Sensa ya watu na makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua, kutathimini na kuchapisha na kusamba...
-
NA. MWANDISHI WETU Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya ...
-
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ametoa siku saba kwa Mkandarasi Kutoka China, China Railway Seventh...
Powered by Blogger.

0 comments:
Post a Comment