METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, October 31, 2016

HAZARD,COSTA WAPELEKA KILIO ST.MARY’S,CHELSEA IKING’ARA UGENINI

chelsea-october-6
Timu ya Chelsea imepata ushindi wake wa ugenini wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Southampton Mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza mechi iliyochezwa katika uwanja wa Mtakatifu wa St.Marry’s.

Wageni walikuwa wa kwanza kuandika bao kupitia kwa Eden Hazard dakika ya sita baada ya kuwachambua mabeki wa Southampton na mfungajia akipiga mpira wa chini chini na kumuacha mlinda mlango Forster akiwa hana la kufanya.

Baada ya kufungwa bao hilo Wenyeji walicharuka na kuliandama lango la Chelsea kama nyuki kutokana na mfumo wa Conte wakutumia wachezaji watano katikati huku nyuma akiweka watatu na kumubakiza mtu mmoja mbele uliwambana vilivyo wenyeji na kushindwa kupenya ngome ya wageni hadi mapumziko Chelsea walikuwa mbele ya bao moja.

Kipindi cha pili kilianza kwa Chelsea kupata bao dakika ya 55 kupitia kwa, Diego Costa baada ya kupokea pasi safi toka kwa kiungo mkabaji Matic huku likiwa bao lake la 7 na kuendelea kuwa kinara wa ufungaji kwenye msimamo wa Ligi hiyo.

Kwa matokeo hayo Chelsea wamepanda hadi nafasi ya nne ya msimamo wakiwa na alama 22 kwa michezo yao kumi wakati Southampton wamebaki nafasi ya tisa na alama 13.

VIKOSI:

SOUTHAMPTON (4-3-3-):Forster; Martina, Fonte, Van Dijk, Bertrand (McQueen 78); Romeu, Clasie (Boufal 61), Davis; Redmond, Tadic (Hojbjerg 78), Austin
SUBS NOT USED: Yoshida, Ward-Prowse, Taylor, Olomola
CHELSEA (3-4-3):Courtois; Azpilicueta, Luiz, Cahill; Moses (Ivanovic 87), Kante Matic, Alonso; Pedro (Willian 78), Costa (Batshuayi 89), Hazard
SUBS NOT USED: Begovic, Oscar, Terry, Chalobah
GOALS: Hazard 6, Costa 55
REFEREE: Mike Jones
ATTENDANCE: 31,827
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com