METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, July 2, 2015

VODACOM KUTATUA TATIZO LA MAWASILIANO CHINI YA ARDHI‏

 

Tatizo la kupata mawasiliano ya simu kwenye vituo vya usafiri vilivyojengwa chini ya ardhi nchini Afrika Kusini limekuwa ni tatizo sugu kwa muda mrefu.Kituo maarufu cha Gautrain ambacho kimekuwa kikitumiwa na wasafiri wengi wakiwemo wanafunzi,wafanyakazi na watalii kwa muda mrefu tangia kifunguliwe mwaka 2010 kimekuwa kikikabiliwa na tatizo la mtandao ambao ulisababisha wasafiri wanaokitumia kituo hicho kushindwa kuwasiliana kwa njia ya simu na barua pepe. 
Kampuni ya Vodacom imejitosa kumaliza tatizo hilo kwa wateja wake ambapo kwa kushirikiana na Idara inayosimamia usafiri wa reli na barabara,uongozi wa kituo cha Gautrain,makampuni ya Bombela na Strategic kwa pamoja makampuni hayo yanafanya mchakato wa kumaliza tatizo la mawasiliano katika kituo hicho.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Ukuzaji Teknolojia wa kampuni ya Vodacom Afrika ya kusini Andries Delport anasema “Siku zote nilikuwa nakerwa na kukosekana mtandao wa mawasiliano ya simu na internet kwenye vituo vya treni vlivyopo ardhini hali ambayo imekuwa ikiwasababishia usambufu abiria.Tunajivunia kuwa mtandao wetu mkubwa nchini Afrika ya Kusini tumeamua kumaliza tatizo hili kwa wateja wetu” 
Tatizo  hili litamalizika kutokana na vifaa bora vya mawasiliano vilivyofungwa na Vodacom  katika vituo vitatu vya treni za ardhini,vifaa hivyo vya kisasa ambavyo ni pamoja na antenna za kurusha mawasiliano zimeunganishwa na mkongo wa mawasiliano uliopo eneo la Rosebank na hatua hii pia itawezesha upatikanaji wa huduma za internet kwa urahisi.
“Utekelezaji huu ni wa awamu ya kwanza tukimaliza hatua hii tutajenga mtandao wa mawasiliano chini ya ardhi  njia yote inayopita treni na kuhakikisha mawasiliano yanakuwa mazuri muda wote,tuko katika mazungumzo ya awali na wadau tutakaoshirikiana nao kutekeelza mradi huu wa kuboresha mawasiliano kwenye miundo mbinu ya usafri iliyojengwa chini ya ardhi”.Alisema Delport.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com