METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, March 6, 2024

KADA WA CCM NEEMA MGHEN ACHANGIA MIFUKO 50 UJENZI WODI YA WAZAZI USHETU

Ushetu, Shinyanga...!

Kada wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Bi Neema Mghen amechangia mifuko 50 ya Saruji yenye thamani ya shilingi milioni 1,150,000/= Kwaajili ya ukamilishaji wa Jengo la wodi ya wazazi katika Zahati ya Sabasabini Halmashauri ya Ushetu.

Akizungumza wakati wa sherehe ya wanawake Duniani ambayo imeadhimishwa katika kijiji cha Sabasabini na jukwaa la Wanawake Halmashauri ya Ushetu huku ikiwa imeambatana na Harambee maalumu kwaajili ya ukamilishaji wa wa wodi hiyo.

Amesema kuwa mkakati huo ni kumuunga mkono Mhe. Rais katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo.

Mgheni amesema, lengo la maadhimisho hayo ni kutoa fursa kwa wanawake na wadau wengine kutafakari changamoto na mafanikio ili kuweka mikakati ya kuwainua wanawake kwa kuwekeza katika miradi mbalimbali ikiwemo Afya Elimu na Miundombinu.

Sambamba na hayo Mgheni amesema ni wajibu wa serikali kupitia Halmashauri kutunga sheria ndogo za kukabiliana na ukatili kwa wanawake na watoto lakini pia kuwaelimisha wanawake juu ya fursa za kiuchumi na wajibu wao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu Hadija Kabojela amesema, Jukwaa la Wanawake Ushetu kwa kutambua umuhimu wa wodi ya wazazi wameona ni vyema kusherehekea siku ya wanawaje dunia kwa kufanya harambee itakayo saidia upatikanaji wa fedha milioni 50 inayohitajika kukamilisha ujenzi wa wodi hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Kata ya Sabasabini Diwani wa viti maalumu Felista Nyerere amesema, wodi hiyo ikikamilika itaondoa usumbufu kwa wanawake ambao wanahangaika sehemu ya kupumzika baada ya kujifungua kwakuwa hakuna sehemu nzuri ya kujifungulia hali inayofanya wakazi wa eneo kwenda umbali mrefu katika kata za Lowa na Bulungwa kutafuta usalama wa mazingira ya kujifungulia.

Harambee hiyo imehudhuliwa na Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Shinyanga Lucy Mayenga aliechangia mifuko 30 ya Saruji, Mbunge wa Ushetu Emmanuel Cherehani ambae amechangia fedha shilingi Milion 1 na Laki tatu, madiwani kupitia baraza lao wamechangia milioni 2 ambapo fedha iliyopatikana kwenye harambee hiyo ni shilingi Milioni 6,482,600 na sarufi mifuko 95 ambapo wodi hiyo itaipewa jina la Neema Mgheni.

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com