METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, March 28, 2023

MBUNGE MASANJA AGAWA MAJIKO YA GESI 700 KWA WANAWAKE WAJASIRIAMALI MWANZA // ATOA SHUKURANI KWA ORYX ENERGIES NA FOMAC





MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja amegawa mitungi ya gesi 700 kwa wanawake wajasiriamali 700 wa Mkoa wa Mwanza lengo ikiwa ni kuhamasisha kuacha matumizi ya nishati chafu ( kuni na mkaa) na badala yake  watumie nishati safi ili kuhifadhi mazingira na pia amekabidhi fedha kiasi cha shillingi milioni 21.

 Hafla hiyo imefanyika leo Machi 27, 2023 katika Ukumbi wa Rocky City Mall jijini Mwanza, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Ndugu Reuben Sixbert Jichabu

 Akizungumza katika hafla hiyo, baada ya kukabidhi majiko kwa niaba ya Mhe. Masanja Bw. Jichabu amewataka wanawake hao kutumia nishati ya gesi ya ORYX katika shughuli zao za ujasiriamali na kuepuka matumizi ya kuni.

Naye, Mhe. Masanja aliahidi kuendelea kuwaunga mkono wajasiriamali wanawake wa Mkoa wa Mwanza ili waweze kukuza uchumi wao.

Aidha Katika Hatua nyingine Mbunge Marry Masanja alizishukuru Kampuni za ORYX na FOMAC kwa kudhamini na kufanikisha tukio hilo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com