METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, August 2, 2022

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AAGIZA WIZARA YA KiLIMO KUFANYA KAZI NA SHIRIKA LA TAIFA LA BIMA

Na Salma Haroun

MAKAMU wa Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt , Philip Mpango ameitaka wizara ya kilimo kufanya kazi na shirika la Taifa la bima ili kuhakikisha wakulima hawapati athari zozote katika kilimo dhidi ya madhara yatokanayo na mbegu zisizo na bora.

Dkt,Philip Mpango ameyasema hayo Agoust 1jijini mbeya wakati akifungua  maonesho ya sikukuu ya Nanenane ambapo amesisitiza suala hilo waweze kulifanyie kazi ili wakulima kuweza kuepukana na changamoto katika kupata mbegu zisizo na bora ambazo husababisha wakulima kupata hasara katika wakati wa mavuno.

Aidha Dkt. Mpango Amelitaka shirika la utafiti Tari kuwa wabunifu katika  kufanya tafiti kwenye mazao mbalimbali yatakayoweza kutumika katika maeneo tofauti kulingana na ardhi iliyopo hapa nchini.

"Kuna mbegu zimeenda kwa wakulima wilaya ya  katavi zimeleta balaaa hazikuzaa  na wakulima wamesema tari imetudanganya turekebishe taasisi  ya tari ya utafiti ili kuleta ubora wa mbegu," amesema .

Kwa upande wake waziri wa kilimo Mh Husseni Bashe, amesema ameziagiza Halmashauri zote wakulima ambao walitakiwa kulipia mbegu za Ruzuku  wasilipie mwaka huu ili kweza kuwapunguzia hasarai walizo zipata mwaka janaa.

Pia Bashe amewataka wakulima waweze kuwa na utayari wa kukabiliana na changamoto  zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa ambapo ni chanzo kimojawapo cha mazao kutokubali katika maeneo yao.

"Wakulima walifundishwa kupanda zao la alizeti wakati wakunyesha mvua na wakati wakulima wamepanda hali ya hewa haikuweza kukubali na kupelekea mazao kuathirika hususani katika nyanda za juu kisini ," amesema.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com