METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, June 23, 2022

SMAUJATA SINGIDA KUYAFIKIA MAKUNDI MAALUM KUYAELIMISHA DHIDI YA UKATILI, WAANZA NA WATOTO WASIO SIKIA

 


Timu ya SMAUJATA ikiongozwa na Mwenyekiti  Bwana Vicent Mafuru wakizungmza na walimu wa shule ya viziwi Tumaini Iliyopo Manispaa ya Singida ili kuanza kutoa elimu ya kukabiliana na ukatili

Wanafunzi wa shule ya viziwi Tumaini wakishangalia kwa furaha wakati wakipata mafunzo walipotembelewa na SMAUJATA mkoa wa Singida. 

Walimu wakifuatilia kikao cha Smaujata Ofisini Kwao mapema hii leo.

Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Singida Akimvalisha Badge ya kampeni hiyo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Tumaini ya watoto wasio sikia

Walimu na Timu ya SMAUJATA wakiwa katika Picha ya Pamoja  baada ya Mazungumzo hii leo

Katibu wa kamati ya Ufuatiliaji ya SMAUJATA Mkoani Singida Bi. Elizabeth Samike akimvisha Beji ya Kampeni hiyo Mkuu wa shule Msaidizi wa Tumaini Rosemary Justine Kiwale.

Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Singida  akimpa mkono Mwalimu Mkuu wa Shule ya Tumaini ya watoto wasio sikia baada ya kumvalisha Beji ya kampeni hiyo shuleni hapo. 


Na Hamis Hussein – Singida

Kampeni ya Shujaa wa maendeleo na Ustawi wa jamii Tanzania SMAUJATA imepanga kuyafikia makundi maalum ya watoto wasio sikia na kuona walioko mashuleni Mkoani Singida kuwapa elimu ya jinsi ya kuripoti na kukabiliana na vitendo vya ukatili katika jamii yao ikiwa ni lengo la kuutokomeza ukatili ili kuwa na jamii endelevu .

Smaujata mkoani hapa imefika katika shule ya  watoto wasio sikia yaani viziwi iliyopo Manispaa ya Singida  na kuueleza uongozi wa shule hiyo juu ya kampeni hiyo ambayo imeanza kuifikia jamii na kuielemisha juu ya ukatili na masuala mbalimbali ya maendeleo baada wiki iliyopita kuzinduliwa rasmi kitaifa.

Akizungumza na viongozi wa shule hiyo ya Viziwi Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Singida Vincent Mafuru alieleza shabaha ya wao kutaka kutoa elimu kwa makundi maalum ya watoto wakiwemo wenye ulemavu wa masikio na macho ambapo alisisitiza kuwa kundi hilo linawezakuwa linakumbana na ukatili lakini likashindwa kutoa taarifa ili kupata msaada.

"Tunahitaji kuyafikia makundi tofauti tofauti,tumeshaanza  mashuleni tumeunda Vilabu vya watoto, tumejaribu kuwaelimisha  namna wanavyoweza kujimudu katika mazingira ambayo ukatili unatokea pia tumelifikia kundi la bodaboda tunawaambia ukatili Sasa ufikie kikomo" alisema Mafuru akiongea na Walimu na wanafunzi wa Shule ya Viziwi Tumaini mkoani Singida.

Kuhusu kuyafikia makundi maalumu ya watoto Mwenyekiti huyo wa Smaujata mkoani Singida  Mafuru alisema kuwa kundi lingine la muhimu kulipatia elimu ya kuripoti na kukabiliana na ukatili ni Kundi la watoto wasio sikia na wale wasioona.

"Tumeona tufike hapa (Tumaini) tuongee na ninyi ili tuone namna ya kuwaelimisha watoto wetu juu ya ukatili unaotendeka kwenye jamii zetu ili waone kuwa mazingira hayo ya ukatili hayana nafasi tena" aliongeza Mafuru.

Mkuu wa shule hiyo ya Tumaini  Mwalimu Francis Damian aliishukuru kampeni hiyo kubisha hodi katika familia hiyo na kusema kuwa elimu watakayoipata watoto itakurahisi hata walimu ambayo ni walezi wa watoto kuweza kuwasiadia pindi wanapofanyiwa ukatili.

"Tunashukuru mmeona na sisi tuko katika jamii, Hawa watoto wanaweza kuwa wanakumbana na ukatili lakini wanakosa mahali pa kuelezea, hivyo elimu hiyo itarahisisha wao kujilinda na hata kama bahati mbaya wamekumbana na ukatili nitakuwa rahisi kwa sisi walezi wao kujua" alisema Mwl.Francis

Mwalimu Francis ametoa siku ya ijumaa ya kila mwezi Smaujata kwenda kutoa elimu ya kukabiliana na ukatili ambapo itakuwa kuanzia saa 10:20 asubuhi hadi saa 12:20 mchana

Kuhusu malezi ya watoto alisema watoto kulala na ndugu wanaowatembelea wazazi ni miongoni mwa sababu inachangia ukatili dhidi ya watoto na kuonyesha kero kwa walezi wenzake wanaofanya ukatili kwa watoto akitolea mfano baadhi ya walimu .

"Watoto kulala na ndugu ambaye amekutembelea nyumbani unakuwa na hofu kwa sababu yanaweza kutokea Yale tunayoyasikia lakini yule Mwalimu aliyewafanyia ukatili wanafunzi ametudhalilisha sana anafundisha huku akiwaharibu, watoto kumbe hata sisi walimu tuna matatizo ,hivyo hakuna mtu wa kumuamini moja kwa moja  kwamba anaweza kumlinda mtoto hiyo elimu hiii  iwe na utashi kwa mapana yake" aliongeza mwalimu Francis.

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com