METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, November 27, 2021

ZAIDI YA WAGONJWA 1141 WA VIKOPE WATIBIWA MKOANI SINGIDA

 

Na Hamis Hussein-Singida

Jumla ya kaya 212,952 kati ya walengwa 212812 sawa na asilimia 100.1 % zimefikiwa na mradi wa vikope kutoka shirika la Hellen Keller International ambapo shirika hilo limezitembelea moja kwa moja kaya hizo kuwabaini  wagonjwa wa vikope kisha kuwapatia matibabu ikiwa ni lengo la  kutokomeza ungonjwa huo kwa mkoa wa singida kwani  ni miongoni mwa magonjwa  makuu matano ambayo hayapewi kipaumbele.

Baadhi ya washiriki wa kikao cha kufunga mradi wa vikope mkoani singida wakisikiliza na kujadiliana mambo mbalimbali.

Mradi huyo uliodumu kwa miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake 2019 ni miongoni mwa jitihada za wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto kupitia mpango wa taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele NTDCP kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ulilenga kupunguza au kuufuta kabisa ungonjwa wa trakoma au vikope ambapo mikoa 20 ikiwemo mkoa wa singida ndiko utekelezaji wake unafanyika ikiwa mradi ambao  unakotekelezwa kupitia shirika la Hellen Keller International kutoka nchini marekani.

 

Mganga mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Viktorina Ludovick amelipongeza shirika hilo kwa namna ambayo limeisaidia serikali na jamii katika kutokomeza  ungonjwa wa trakoma alipokuwa akizungumza na washiriki wa kikao cha ufungaji wa mradi huo kumwakilisha katibu tawala wa mkoa.

 

 “Kwa kushirikia na timu zetu za mikoa na halmashauri pamoja na mdau wetu Hellen Keller International tumeweza kutekeleza mpango wa kutokomeza vikope kwa Halmashauri zeto sita  Manyoni , Itigi Ikungi Mkalama Singida Vijijini na Singida Manispaa  jumla 212952 kati ya walengwa 212812 sawa na 100.1% . Hapa tunaona uhitaji ulikuwa mkubwa na tumetekelea mpaka tumevuka lengo”.  amesema Dr Ludovick 

 

Mganga Mkuu mkoa wa singida Dr. Viktorina Ludovick akizungumza na washiriki wa kikao cha kufunga  mradi wa vikope kutoka shirika la HKI katika ukumbi wa Aqua Vitae Resort Singida.


Ameyataja mafanikio mengine kuwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya kubaini na kutibu wagonjwa wa vikope wataalamu wawili ngazi ya mkoa, wataalamu 13 ngazi ya halmashauri, wahudumu wa afya 1308 ngazi ya kata na vijiji pamoja na wahudumu afya 2851 ngazi ya jamii.

Dr Ludovick ameongeza kuyataja mafanikio kupitia mradi wa vikopte kutoka shirika La Hellen Keller Interentaional kuwa wagonjwa 1141 wa vikope ambao walikuwa na tatizo hilo aidha  bila kujua au  kukosa sehemu ya kupata msaada walipata huduma.

 

Meneja mradi wa trakoma kutoka shirika la Hellen Keller International (HKI) Athuman Tawakal amesema lengo kubwa la kuleta mradi huo ilitokana na takwimu zilizoonyesha uhitaji wa huduma hizo kwa waathirika wa ugonjwa wa vikope.

“ Tumekuja katika maeneo haya  baaada ya kupata takwimu kutoka wizara ya afya kuonyesha ukubwa wa ugonjwa huu wa trakoma  katika maeneo haya na tuliagizwa na wizara kupitia mpango wa kutokomeza magonjwa yasiopewa kipaumbele ili kusaidia halmashauri  na mkoa  katika kuwatafuta wagonjwa na kuwapatia matibabu na tumeweza kufanikiwa . tumeweza kuwasidia watanzania zaidi ya 1100 kuwapatia matibubu na tumekuwa tukifanya ufutiliaji”.

 

Meneja mradi kutoka shirika la HKI Athuman Tawakal Akizungmza na washiriki wakati wa kufunga mradi wa vikope mkoani singida tangu ulipoanzishwa 2019


Dr. Julius Nyenje mratibu wa magonjwa yasiopewa kipaumbele kutoka wilaya ya Mkalama amelishukuru shirika la HKI kwa kuwajengea uwezo wa mapambano dhidi ya ungonjwa wa trakoma.

“Trakoma au ungonjwa wa vikope ilikuwa moja ya  magonjwa  makuu matano ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele na HKI mmechukua nafasi kubwa sana  na jamii yetu imepata huduma njema .tunawashukuru sana”. alisema dr. Julius mratibu wa magonjwa yasiopewa kipaumbele kutoka wilaya ya Mkalama.

Mratibu wa magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele kutoka wilaya ya Mkalama Dr. Julius Nyenje akitoa shukrani kwa shirika la Hellen Keller International wakati wa kufunga mradi wa vikope .


Fatuma Jumapili, Elizabeth Wilbroad na Shabani Hamisi  ni Baadhi ya wanufaika wa mradi wa vikope kutoka shirika la HKI wamesema huduma ya matibabu ya vikope imewasaidia sanaa kurejesha uwezo wao wa kuona na kulipongeza shirika hilo kwa namna lilivyotekeleza mradi huo.

 

Dr Upendo Mwakabalile mratibu wa huduma za macho mkoa wa singida amewasisitiza wataalamu wengine waliopata mafunzo ya namna ya kuwahudumia  wagonjwa wa vikope kutunza takwimu ili ziweze kusaidia baaadae na kuwataka elimu waliopata kuifanyia kazi kwa watu wengine wenye uhitaji.


“Naomba kila mtu azingatie sana kwa sababu pasipotakwimu kazi yetu tulioifanya kwa miaka mitatu itakuwa imepotea, kwahiyo takwimu inakuwa ni ushahidi. hawa wahudumu 13 tuliopewa mafunzo tusipofanyia kazi hiyo elimu yetu itakuwa sawa na bure”.  
amesema Dr. upendo

Mradi wa vipoke mkoani singida umetekelezwa na shirika la Hellen Keller International ikiwa ni miongoni mwa jitihada za wizara ya afya  maendeleo ya jamii  jinsia wazee na watoto kupitia mpango wa  taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele NTDCP kwa kushirikiana na timu za mikoa na wilaya  na wadau mbalimbali ambapo mradi umetekelezwa kwenye wilaya sita ambazo  ni manyoni , itigi , ikungi ,mkalama , singida manispaa na singida  vijijini  ambazo ziliathiliwa na ungojwa wa vipoke kwa kiwango kikubwa .





 

 

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com