Katibu Mkuu Wizara ya
Kilimo Bwana Gerald Kusaya akisaini kitabu cha Wageni kabla ya kuanza kikao
kifupi na Viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Karagwe.

Katibu Mkuu
Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya leo tarehe 12 Agosti, 2020 ameweka bayana
kutilia shaka mienendo ya Viongozi na Watumishi wa Chama Kikuu cha Ushirika cha
Karagwe na Kyerwa (KDCU) wakati wa mkutano wake na Viongozi na Watumishi hao
katika ukumbi wa makao makuu ya Chama hicho Kikuu, wilayani Karagwe.
Katibu Mkuu
Kilimo Bwana Gerald Kusaya amesema katika taarifa za awali kutoka kwa wasamalia
wema zimeonyesha kuwa kuna tuhuma; Kuwa kuna baadhi ya Wanunuzi wa kahawa,
wamekuwa wakitoa rushwa ili wauziwe kahawa kwa bei ya chini; Jambo ambalo
linachangia kuwadhulumu Wakulima haki yao ya kupata bei nzuri.
Katibu Mkuu
Kilimo Bwana Kusaya amemtaja Mnunuzi mmoja wapo kuwa ni Mmiliki wa Kampuni ya
Mambo Coffee; Kuwa amekuwa mstali wa mbele katika utekelezaji wa jambo hilo.
Bwana
Kusaya ameongeza kuwa kwa nyakati tofauti Viongozi na Watumishi wa KDCU
wamekuwa wakipokea fedha kwa njia ya simu na kwenye akaunti zao za Benki,
Ikidhaniwa kuwa ni kwa ajili ya kutekeleza nia ovu ya kushawishi na kutoa
upendeleo kwa Wanunuzi binafsi.
Katibu Mkuu
Kusaya alimtaja Mhasibu Mkuu wa KDCU Bwana Juvenary Burchard, Mtumishi mwengine
ni Bwana Oscar Dominick Mjuni aliwekewa fedha kiasi cha shilingi milioni 1 saa
2:07 usiku wa tarehe 12 Machi, 2020 na tarehe 14 Machi, 2020 aliwekewa tena
kiasi cha shilingi milioni 1, Mtumishi mwengine aliyefahamika kwa jina moja Bi.
Whitney ambapo, tarehe 1 Aprili, 2020 saa 8:01 mchana aliwekewa kiasi cha
shilingi milioni 2.4.
Watumishi
hao watatu kwa nyakati tofauti walipoulizwa fedha hizo zilitumwa kwako kwa
lengo gani; Wote hawakusema.
Taarifa
hiyo ya Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo pia haikumuacha salama Mkuu wa wilaya ya
Karagwe Mhe. Godfrey Mheluka ambaye naye kwa wakati mmoja alipokea fedha kiasi
cha shilingi milioni 1 kutoka kwa Mnunuzi wa kahawa wilayani humo na hata
alipoulizwa lengo la kutumiwa fedha hizo na hakusema fedha hizo alitumiwa kwa
lengo gani.
Katibu Mkuu
Kusaya aliagiza Viongozi na Watumishi hao wa KDCU kuwasilisha taarifa zao za
Benki (Bank Statements) kuanzia Januari, 2020 hadi Mwezi Agosti, 2020 na kwamba
zimfikie ofisini kwake Dodoma tarehe 30 Agosti, 2020.
Awali
Katibu Mkuu Kilimo Bwana Gerald Kusaya alitaka kufahamu taarifa ya kupotea kwa
fedha kiasi cha shilingi bilioni 5.7; Akijibu swali la Bwana Kusaya, Meneja wa
KDCU Bwana Oscar alianza kwa kusema fedha zilizopotea ni shilingi bilioni 3.4
na si 5.7 na kuendelea kumfahamisha Katibu Mkuu kuwa ufisadi huo ulitokea mwaka
2014 na kuongeza kuwa hii ni Bodi ya Viongozi wa Awamu ya Nne na kwamba hawahusiki na kutoa maelezo kuwa usahihi wa deni hilo unaweza kufahamika
kuanzia mwaka 2014 kurudi nyuma.
Katika
hatua nyengine Katibu Mkuu Kusaya alidokeza kuwepo kwa taarifa za kutia shaka
kuhusu uwezo wa kifedha wa Meneja wa KDCU Bwana Oscar Dominick ambapo kuna
tuhuma kuwa anamiliki hotel inayojulikna kwa jina la Toronto.
“Kuna
taarifa kuwa Bwana Oscar unamiliki hotel inayoitwa Toronto, wewe kama Kiongozi
wa Umma naamini ulijaza fomu ya tamko la mali; kila kila sababu ya kuulizwa na
kudhibitisha ulipata wapi hizo fedha za kujenga hiyo hotel, kabla ya kuwa
Kiongozi wa KDCU au ulizipata wakati ulipokuwa Kiongozi na ulizipataje?.”
Amekaririwa Bwana Kusaya.
Katibu Mkuu
Kusaya wakati wa mazungumzo yake aliuliza kuhusu ukaguzi uliopita kwa Chama
hicho Kikuu cha KDCU ambapo Bwana Oscar Dominick alisema Chama kilipata hati
yenye mashaka na kusema sababu kuwa ni kuchelewa kuwasilisha taarifa ya benki
(Certified Bank Statement) ambayo ingeonyesha kama Chama hiko Kikuu ch Ushirika
kilimaliza kulipa deni lake kutoka Benki ya Kilimo (TADB). Fedha hizo zilikopwa
ili kulipa madeni ya Wakulima wa zao la kahawa.
Katibu Mkuu
Bwana Gerald Kusaya amewaonya Viongozi wa Chama Kikuu cha KDCU na kuwakumbusha
maneno ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kaasim
Majaliwa kuwa; kama kuna Kiongozi ambaye amechaguliwa kuwa Kiongozi kwenye
Chama cha Ushirika akiamini kuwa kwa kuwa atawaibia Wanachama na akatajirika
haraka haraka, aache mawazo hayo. Ushirika wa sasa hautawavumilia Viongozi wezi
na wabadhilifu.
Aidha
katibu Mkuu amewaagiza Viongozi wa Chama Kikuu cha KDCU kuanza mara moja
mchakato wa kununua mizani bora na ya kisasa kwenye AMCOS ili kuondoa kero ya
Wakulima kulalamikia kuibiwa mazao yako.
“Kumekuwa
na malalamiko kutoka kwa Wakulima kwenye zao la kahawa na korosho, wanapopima
kwenye AMCOS zao na baadae wanapopeleka kwenye Chama Kikuu kuna kuwa na
utofauti wauzito, hatuihitaji tena kusikia tofauti za mizani”
Nafaham
KDCU ina AMCOS zaidi ya 100; Anzeni kununua kwa awamu baadae mtakuwa mmetimiza lengo la kununua
mizani kwa AMCOS zenu zote.
“Wito wangu kwenu KDCU pangeni mipango vizuri na hakikisheni msimu wa ununuzi wa zao la kahawa; mnalipa madeni yote ya Wakulima, ingie msimu mwengine bila ya kuwa na madeni, Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli hataki kusikia kero za aina hii”. Amekaririwa Katibu Mkuu.
0 comments:
Post a Comment