METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, August 1, 2020

KM Kilimo-Gerald Kusaya azitaka Taasisi za Kilimo Zinazoshiriki maonesho ya Nane Nane kufikisha Teknolojia kwa Wakulima

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw Gerald  Kusaya akikagua mifuko maalumu ya kuhifadhia nafaka unaomwezesha mkulima kuhifadhi nafaka kwa muda mrefu bila kuharibika. (Picha zote na Innocent Natai)

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw Gerald  Kusaya,akisikiliza maelezo kutoka kwa mtaalam wa Taasisi ya TPRI,Taasisi inayojishughulisha na utafiti wa Vuatilifu na visumbufu vya mimea na mazingira.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw Gerald  Kusaya,akisikiliza maelezo kutoka kwa mtaalam wa Taasisi ya TPRI,Taasisi inayojishughulisha na utafiti wa Vuatilifu na visumbufu vya mimea na mazingira.

Na Innocent Natai, TPRI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw Gerald Kusaya amezitaka Taasisi zilizopo chini ya Kilimo zinazoshiriki maonesho ya nane nane  kuhakikisha teknolojia wanazozionyesha katika maonesho hayo zinawafikia wakulima kwa wakati,

Hii ni ili kuwasaidia kuondokana na Kilimo cha kubahatisha au cha mazoea,Ameyasema hayo alipokuwa akitembelea mabanda ya Taasisi hizo katika maonesho hayo yaliyozinduliwa mapema hivi leo Bariadi mkoani Simiyu

Kusaya amesema upo umuhimu wa kuwapa elimu na teknolojia mpya wakulima kwani wamekuwa wakilima Kilimo kisicho na tija angali kunataasisi za utafiti zinazozalisha teknolojia bora zitakazo weza kuwasaidia wakulima kuondokana na aina hiyo ya kilimo

Ameongeza kuwa Kilimo sasa kimekuwa tena sio cha watu wasio na na elimu au wasio na ajira bali kimekuwa ndio mhimili mkuu wa taifa hasa katika kipindi hichi Taifa linapoelekea katiaka uchumi wa viwanda kwani viwanda vinategemea malghafi kutoka katika kilimo

Kusaya ameongeza kuwa dhumuni la maonesho hayo kufanyika kila mara sio tu kuonyesha na kushiriki bali ni kuhakikisha kazi zinazofanywa na Taasisi hizo za Kilimo,Mifugo na Uvuvi zinaonyeshwa na kuwafikia wakulima eidha kwa elimu au vifaa 

pia Bw Kusaya ameitaka Taasisi ya TPRI kuendelea kudhibiti Viuatilifu visivyo kidhi vigezo kuingia au kutumiaka hapa nchini kwani vimekuwa ndio sababu nyingine ya wakulima wengi kupata hasara katika Kilimo na hatimae kukimbia katika tasnia ya Kilimo

Aidha pia ameutaka uongozi wa Tume ya Vyuo Vikuu vya Kilimo kuhakikisha wanatoa elimu kwa vitendo kwa wanafunzi ili kuhakikisha wanapomaliza elimu zao wanakwenda vijijini kuwasaidia wakulima

Maonesha hayo ya nane nane yamezinduliwa hivi leo kitaifa hapa Bariadi Mkoani Simiyu,mgeni rasmi akiwa ni Makamu wa Rais Mhe Samia Suluh Hassan na yanatarajiwa kufungwa rasmi tarehe 8/8/2020 Ambapo ndio siku ya kilele mgeni rasmi akiwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Mwisho.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com