Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mkoani humo, kabla ya kufunga kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi hao ambayo ilikuwa ikiendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, kwa lengo la kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha Sita wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(hayupo pichani) akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mkoani humo, kabla ya kufunga kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi hao ambayo ilikuwa ikiendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa kwa lengo la kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.
Afisa Afya wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Reuben Malimi akitoa elimu ya tahadhari dhidi ya Homa ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Korona kwa wanafunzi wa kidato cha Sita mkoani humo waliokuwa katika kambi ya Kitaaluma shule ya Sekondari ya Wasichana ya Maswa, kabla ya kambi hiyo kufungwa ili kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha Sita wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(hayupo pichani) akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mkoani humo, kabla ya kufunga kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi hao ambayo ilikuwa ikiendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa kwa lengo la kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.
Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akitoa taarifa ya hali ya kambi ya kitaaluma kwa waanfunzi wa kidato cha sita mkoani humo, kabla ya kumkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini kuzungumza na wanafunzi hao, kabla ya kufunga kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi hao , ambayo ilikuwa ikiendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, kwa lengo la kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.
Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umefunga kambi ya Kitaaluma kwa
wanafunzi wa kidato cha Sita mwaka 2020 iliyokuwa ikifanyika katika Shule ya
Sekondari ya Wasichana Maswa , ikiwa ni sehemu ya tahadhari dhidi ya Homa kali
ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona.
Akifunga kambi hiyo, Machi 16, 2020 Katibu Tawala wa
Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema uongozi wa mkoa umefikia hatua hiyo
kuchukua tahadhari kama ilivyoelekezwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa juu ya
kuzuia mikusanyiko ya watu wengi isiyo ya lazima katika kipindi hiki ambacho
kumeripotiwa idadi ya watu kadhaa kubainika kuwa na virusi vya Corona katika
nchi mbalimbali.
“Kutokana na Maelekezo ya Serikali Mkoa umeona kambi hii
ifungwe kwa ajili ya tahadhari dhidi ya Corona, Mhe. Rais amesitisha mbio
za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2020, Mhe. Waziri Jafo amesitisha UMISETA na
UMITASHUMTA na tahadhari mbalimbali zimeendelea kutolewa na Serikali ikiwemo ya
kuzuia mikusanyiko; sisi hapa tuna wanafunzi takribani 1000 kutoka shule
10 hivyo tumekubaliana kwa pamoja tuifunge kambi hii,” alisema Sagini.
Aidha, Sagini amesema pamoja na kambi za kitaaluma kufungwa
Mkoa utaendelea kusimamia utekelezaji wa mkakati wa taaluma wa mkoa ili walimu,
wanafunzi na wadau wengine wa elimu waweze kutimiza wajibu wao kuhakikisha Mkoa
unatimiza adhma yake ya kuwa miongoni mwa mikoa itakayofanya vizuri katika
mitihani yote ya Kitaifa.
Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest
Hinju amesema wanafunzi hao walitakiwa kukaa kambini muda wa wiki sita kwa
ajili ya maandalizi ya Mtihani wa Taifa unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei 2020,
hivyo pamoja na kusitisha kambi hiyo walimu wamehimizwa kutimiza wajibu wao
katika ufundishaji na wanafunzi wametakiwa kwenda kusoma kwa bidii ili kufikia
lengo la Mkoa.
Awali akitoa elimu ya ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa
na virusi vya Corona kwa wanafunzi na walimu kabla ya kambi kufungwa, Afisa
Afya wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Reuben Malimi amesema ugonjwa huo hauna tiba
matibabu yanayofanyika yanazingatia dalili zinazoonekana kwa mgonjwa, hivyo ni
vema kila mmoja akachukua tahadhari kwa kuzingatia maelekezo na elimu
inayotolewa na wataalamu wa afya katika maeneo mbalimbali.
Nao wanafunzi wa Kidato cha Sita wa Mkoa wa Simiyu
wameshukuru uongozi wa Mkoa kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona kwa
kutoa elimu kuhusu Corona kabla ya kufunga kambi, huku wakieleza namna
ambavyo kufungwa kwa kambi kunaweza kuathiri malengo yao waliyojiwekea.
“Tunashukuru uongozi wa Mkoa kutoa elimu na kuchukua
tahadhari ya Corona kwa kufunga kambi ni hatua ya kutuhakikishia usalama, lakini
kambi ilitusaidia kujua namna ya kujibu maswali ya mtihani wa Taifa na
kujifunza mada ngumu tulizoshindwa shuleni kupitia kwa walimu mahiri, tutatumia
muda huu kujisomea kwa bidii ili tufaulu vizuri mtihani wa Taifa,” alisema
Isack Ndassa kutoka Shule ya Sekondari Kanadi Itilima.
0 comments:
Post a Comment